MWANAMKE MAKINI BLOG

Advertise Here

Sunday 2 November 2014

PIGO KURA ZA MAONI CCM YAKATIKA KWA KIKWETE



MCHAKATO wa Chama cha Mapinduzi CCM kumpata mgombea uenyekiti wa kijiji cha Kihangaiko tarafa ya Msata Wilayani Bagamoyo mwishoni mwa wiki umeiingia dosari baada ya wajumbe wa mkutano huo kunusurika kuzichapa hadaharani wakati kila kindi likitaka mgombea wake apite.

Ngumi zilibuka mkutanoni hapo baada ya msimamizi wa uchaguzi huo kutoka Kata hiyo Adamu Kitegire akiungwa mkono na wana-ccm kutoka tawi la Madesa kutangaza kuahilisha mkutano huo na kuzichoma moto kura zilizokuwa zimepigwa kuwachagua wajumbe wa serikali kwa madai kuwa wanachama waliopiga kura hizo hawakuwa halali.

“naahirisha mkutano huu wa mchakato kupata wagombea hadi hapo itakapopangwa tena,sababu kubwa ni kuwa kwanza wengi wenu hapa sio wanachama halali wa CCM hivyo hatuwezi kuendelea”alisikika Kitegire.

Kufutia makauli hiyo nae mwenyekiti wa ccm tawi la Kihangaiko Mohamedi Kisulu akiungwa mkono na wanachama wake alikataa na kumtuhumu msimamizi wa uchaguzi huo kuwa anakusudia kuweka viongozi wake kwa masilahi binafsi badala ya wanaopendekezwa na wanachi.

Hata hivyo baada ya taflani iliyodumu kwa takribani nusu saa Mwenyekiti Kisulu alizira kikao na kuondoka zake akiwaacha wajumbe wamkutano huo wakiwa wamechachamaa wakishutumiana kwa maneno makali yakiwemo ya ubaguzi wa uzawa na kushikana mashati.

Kumegeka kwa wana ccm kulienda mbali zaidi baada ya wanachama kutoka Madesa kutamka wazi wazi kuwa kama mgombea wao hata pita basi watakiua chama kwa kumchagu kiongozi kutoka upinzani na hatakama atashinda mgombea wa chama hicho basi hawatashirikiana nae hadi atakapoondoka madarakani.

“kwanza mgombea wenu ‘Madesa’ Eliazari Kaloli mmempitisha kwa rushwa,iweje kura ziwe nyingi kuliko wajumbe wa mkutano halafu mnataka mmpitishe...tunasema akipita tunakiua ccm kwa kuwaunga mkono upinzani”alisema Selemani Juma.

Huu ni mchakato kumpata mgombea uenyekiti na wajumbe wa halamashauri ya kijiji ndani ya chama cha mapinduzi CCM ikiwa ni hatua ya kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa tarehe 4/12/2014 ambapo wateule katika chama hicho watakutanishwa na wateule wa vyama vingine ili kumpata mwenyekiti.

No comments:

Post a Comment