MWANAMKE MAKINI BLOG

Advertise Here

Tuesday 4 November 2014

MKUTANO WA 16 & 17 BUNGE LA JAMHURI WAANZA LEO



MKUTANO wa kumi na sita na wa kumi na saba wa bunge la jamuhuri ya muungano wa Tanzania umefanyika mjini Dodoma.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Bunge,
Idara ya Habari, Elimu kwa Umma na Uhusiano wa Kimataifa,
Mikutano hiyo haikufanyika kwa wakati uliopangwa kutokana na kuwepo kwa bunge maalumu la katiba.

Taarifa hiyo imeeleza kwamba mikutano hiyo yote miwili sasa itafanyika kuanzia tarehe 4 hadi 28 mwezi huu.

Kazi zitakazofanyika katika mikutano hiyo ni pamoja na Bunge kukaa kama Kamati ya Mipango kwa mujibu wa masharti ya Kanuni ya 94(1) na kupokea, kujadili na kutoa maoni na ushauri kuhusu bajeti ya serikali, vyanzo vya mapato pamoja na mapendekezo ya utekelezaji wake.

Aidha kutakuwa na kusomwa kwa mara ya pili na hatua zake zote kwa miswada ya Sheria ya Serikali ambayo ilikwishasomwa kwa mara ya kwanza katika mikutano iliyotangulia; Muswada Binafsi wa Mbunge na Muswada Binafsi wa Kamati

Miswada itakayosomwa kwa mara ya pili ni Muswada ya Sheria ya Kodi ya Ongezeko la Thamani wa Mwaka 2014, Muswada wa Sheria ya Takwimu  wa Mwaka 2013, Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Ubia baina ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi  wa Mwaka 2014  na, Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria mbalimbali  wa Mwaka 2014.

Aidha, kutakuwa na maswali ya kawaida kwa mujibu wa kanuni ya 39 (1) ambapo kwa mikutano hii miwili yatakuwa 265 na  maswali kwa Waziri Mkuu kwa mujibu wa kanuni ya 38(1).

No comments:

Post a Comment