MWANAMKE MAKINI BLOG

Advertise Here

Saturday 8 November 2014

WAZIRI MEMBE AIKINGIA KIFUA CHIDA MADAI DHIDI WIZI PEMBE ZA NDOVU



WAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa mheshimiwa BERNAD MEMBE  ameutaarifu umma wa watanzania na dunia kwa ujumla kwamba madai yaliyotolewa na taasisi isiyo ya kiserikali ya nchini  Marekani ya Environmental investigation Agency EIA hayana ukweli wowote.

Pia  amekanusha madai yamkwamba serikali ya Tanzania haijali na wala haichukui hatua dhidi ya wanaojishughulisha na biashara haramu ya pembe za ndovu.

Akitoa tamko la serikali kuhusiana na shutuma iliyotolewa na taasisi hiyo dhidi ya serikali ya Tanzania leo bungeni mjini Dodoma mheshimiwa MEMBE amesema taarifa hizo zote ni za kupikwa na kuungwa mkono ili kuchafua heshima ya Tanzania na heshima ya Taifa la China.

Ametaja sababu za kusema taarifa hizo ni za uongo kuwa taarifa kama hiyo sio mara ya kwanza kutolewa iliwahi kutolewa mwaka jana na mtoa taarifa ambaye ametajwa kuwa chanzo cha habari ni mtu mmoja ambaye walimkuta barabarani na kuanza kumuuliza maswali ilhali sio sio mtumishi wa bandari wala uwanja wa ndege.

Mbali na hilo amesema ziara ya rais huyo wa China ilikuwa ya masaa 24 na programu yake ilianza mara tu alipowasili nchini kuanzia saa 9 alasiri hadi saa 4 usiku kwenye dhifa  ya Taifa na kuhoji hizo shopping zinazoelezwa kufanywa na ujumbe wa rais huyo zilifanywa muda gani.

Mheshimiwa MEMBE amewataka watanzania kutokubali upuuzi wa aina hiyo kwa kuwa Tanzania ni Taifa huru halichaguliwi marafiki wala halirithishwi maadui na kuahidi kuendeleza ushirikiano uliopo wa kidugu na China na kwame hawarudi nyuma kutokana na maneno ya uwongo na uzushi.

Jana vyombo vya habari vya ndani na nje ya nchi vilito habari kwamba ujumbe wa rais wa China uliokuja nchini mmiezi 18 iliyopita ulijihusishq na ununuzi wa pembe za ndovu nchini chnazo cha habari kikiwa ni kutoka kwa Taasisi hiyo ya EIA.

No comments:

Post a Comment