MWANAMKE MAKINI BLOG

Advertise Here

Friday 7 November 2014

AJALI MBAYA YA BASI NA TRENI YAUA 12 NA KUJERUHI 44



·  WATU 12 wamefariki na wengine kadhaa 44 kujeruhiwa baada ya basi walilokuwa wakisafiria kugonga garimoshi katika eneo la Kiberege Tarafa ya Mangula Wilaya ya Kilombero mkoani Morogogro. 

Kamanda wa polisi mkoa wa Morogoro Leonard Paulo amesema kuwa basi hilo Kampuni ya SUPER ALJABIR lenye Namba za usajili T.725 ATD SCANIA BUS lililokuwa likiendeshwa na KASIM NDELA (35) mkazi wa Morogoro, liligonga garimoshi lililokuwa likisafiri kutoka Mbeya kwenda Dar es Salaam wakati dereva alipojaribu kuvuka reli. 

Waliofariki ni pamoja na wanaume 6 wanawake 4 na wasichana wawili wenye umri kati ya miaka 5 na 6.

Hata hivyo Kamanda Paul amesema kuwa majeruhi 24 wametibiwa na wameruhusiwa, ambapo 20 waliobaki kati yao ni wanawake 15 wanaume wane na mtoto mmoja.

No comments:

Post a Comment