MWANAMKE MAKINI BLOG

Advertise Here

Tuesday 4 November 2014

DAWASCO YAPOTEZA 56% YA MAJI HOLELA



ASILIMIA 56 ya maji yanayozalishwa na kusambazwa na Mamlaka ya Maji Jijini Dar es Salaam (DAWASCO) yanapotea bila kulipiwa  imeelezwa.

Kauli hiyo imetolewa leo mjini Dodoma na Waziri wa Maji Profesa Jumanne Maghembe alipokuwa akifungua mkutano wa 15 wa Mamlaka ya maji mijini.

Maghembe amesema upotevu huo wa maji umekuwa ukifanywa na baadhi ya watendaji wa mamlaka hiyo na hivyo kuikoasesha mapato.

Amesema hivi sasa DAWASCO imekuwa ikipata mapato ya jumla ya shilingi. Bilioni 3.5 kwa mwaka lakini endapo maji hayo yangekuwa yakiwafikia wateja wote  wangeweza kupata zaidi ya hapo.

Waziri Maghembe amesema ni vyema sasa mamlaka zote nchini zikahakikisha kuwa maji hayapotei na yote yanayozalishwa yanawafikia walengwa.

Amesema ni muhimu kutafuta teknolojia ambayo itabaini upotevu huo wa maji mapema ili kudhibiti maji na kuongeza mapato kwa mamlaka.

Amesema kwa upande wa Jiji la Dar es Salaam Wizara ina mpango wa kuhakikisha kila mteja anafungiwa mita ya maji kwa ajili ya kuhakikisha kuwa analipa maji kadri anavyotumia.

Awali akimkaribisha Waziri kufungua mkutano huo, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dk Rehema Nchimbi amesema ni vyema mamlaka zinzoambatana katika utuoaji wa huduma zikawa zinashirikiana katika kutoa huduma kwa wananchi.

No comments:

Post a Comment