MWANAMKE MAKINI BLOG

Advertise Here

Thursday 13 November 2014

NHIF YATUMIA BIL.36 KUKAMILISHA KITUO CHA UCHUNGUZIN MATIBABU


KITUO cha Kisasa cha Uchunguzi na Matibabu ya magonjwa ya binadamu kinachojengwa katika Chuo Kikuu cha Dodoma UDOM kipo katika hatua za mwisho mwisho za ukamilishwaji.

 
 Kituo hiki kitahudumia wagonjwa kutoka maeneo mbalimbali ya mikoa ya jirani ya na mkoa wa Dodoma na kinajengwa kwa ufadhili wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya NHIF kwa gharama ya shilingi Bilioni 36 ambazo zimetolewa na mfuko huo kwa  silimia 100.


Akizungumza na wahariri wa vyombo mbalimbali wanaohudhuria kongamano la Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya linalofanyika kwenye hoteli ya Dodoma mjini humo walipotembelea na kujionea maendeleo ya ujenzi wa kituo hicho, Kaimu Mkuu wa Chuo hicho Profesa Mlacha Shaaban amesema “Kituo hiki kitajikita zaidi kwenye magonjwa ya uchunguzi na utafiti  pia kitatoa wataalamu kutoka katika kitivo cha afya cha Chuo kikuu cha UDOM.


Shaaban amesema wataalamu watakaofanya kazi katika kituo hicho watakuwa wakifundisha wanafunzi na kuhudumia katika kituo hicho, Kituo hicho kinatarajiwa kuanza kutoa huduma ifikapo Januari 2015.

No comments:

Post a Comment