MWANAMKE MAKINI BLOG

Advertise Here

Friday 7 November 2014

MAHAKAMA ZA MWANZO MARUFUKU KUAMUA MASHAURI YA ARDHI



·    SERIKALI, imezipiga marufuku Mahakama za Mwanzo kuamua mashauri ya kesi za Ardhi kwani jukumu hilo ni la Mabaraza ya Ardhi ya Wilaya.

Onyo hilo limetolewa na Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Angellah Kairuki, wakati alipokuwa akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Nkenge, Assumpter Mshama (CCM), lililoulizwa kwa niaba yake na Mbunge wa Mwibara, Alphaxard Lugola (CCM).

Mbunge huyo ametaka kujua kwanini serikali isitoe kauli na tamko la kuwataka Mahakimu wa Mahakama za Mwanzo kutopokea kesi hizo na badala yake izipeleke kwenye mabaraza ya ardhi.

Pia ametaka kujua ni kwani serikali isibebe mzigo wa kuwafidia watu waliopata hasara kutokana na ucheleweshwaji wa kesi uunaofanywa na Mahakama hapa nchini.

Katika swali la msingi, alitaka kujua sababu zinazopelekea kesi ikae Mahakamani zaidi ya siku zilizowekwa.

Amesema, kukomesha tabia ya mahakama za Mwanzo kuhukumu kesi la Ardhi serikali itawasiliana na Makama za mwanzo ili ziweze kuchukua hatua stahiki katika jambo hilo.

Kuhusu, ucheleweshwaji wa kesi taratibu  zinafahamika kwa wale ambao watakuwa na sababu za msingi lakini mahakama zimekuwa haziahirishi kesi bia sababu yoyote endapo itakuwa kusababu zimeeleweka kamati za mahakimu na za majaji wataweza kufuatilia na kuchukua hatua.

No comments:

Post a Comment