MWANAMKE MAKINI BLOG

Advertise Here

Thursday 11 December 2014

AJALI YAUA MMOJA ENEO LA MAGUZONI BARABARA KUU TANGA-SEGERA

·    MTU mmoja Jeremia Steven Mshana (54) mkazi wa Tangasisi Wilayani Tanga mjini amefariki katika ajali iliyohusisha Gari NO.T.413 SCX aina ya SUZUKI CARRY aliyokuwa akiendesha kugongana na gari mali kampuni ya Hajees yenye namba za usajili T.935 aina ya BUW YOUTONG BUS.

Imefahamika kwamba Hajeez ilikuwa ikiendeshwa na Omari Nguku  mwenye umri wa miaka  38 mkazi wa Tanga Mjini wakati akitokea Arusha kuja Tanga.

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoani  Tanga Frasser Kashai amesema ajali hiyo imetokea mnamo  Desemba 10 mwaka huu majira ya saa 10:15 jioni  eneo la Maguzoni Kata ya Songa Tarafa ya Mbwembwela Wilaya ya Muheza. Marehemu alikuwa akitokea Tanga kuelea Segera.
Aidha Chanzo cha ajali hiyo  ni kutokana na Dereva wa Bus kuhama upande wake, na Kamanda Kashai amesema dereva huyo amekamatwa na atafikishwa mahakamani  kujibu tuhuma inayomkabili.

No comments:

Post a Comment