MSHAURI wa mradi wa
kitaaluma kutoka nchini Finland Tero Tapani amewataka watanzania kuwasaidia, kuwajali
na kuwatahamini watoto yatima na
walemavu kwani watoto wote ni sawa na wana nahaki ya kuishi kama wengine.
Tpani
alikuwa akizungumza katika sherehe ya watoto yatima na walemavu ambayo
imefanyika katika ukumbi wa mkutano YDCP Desemba 2, mwaka huu Jijini Tanga.
Amesema
jambo bora na lenye Baraka ni kuwathamini watoto mlemavu na kuwatunza, kwani hata
kristo aliagiza kuwaacha watoto waende kwake kwa kuwa kuna siri nyingi za
ufalme wa Mungu.
Mratibu
wa kituo cha YDCP, William Henry amesema kuwa lengo la kuadhimisha sikukuu hiyo
ya watoto kila mwaka ni kuwaweka pamoja ili wajisikie vizuri kama watoto
wengine.
Naye
Mch. Ayubu Kuminambili wa kanisa la Free Pentekoste Of Tanzania (FPCT) ambaye
alimwakilisha makamu Askofu wa kanisa hilo nchini Stivie Mulenga amesema kuwa
amdharauliye wenzake atenda dhambi bali amhurumiaye mwenzake ana heri, hivyo ni
vyema kuwapenda watoto walemavu na kuwatunza kwani Mungu amewaumba kwa makusudi
maalum.
No comments:
Post a Comment