MWANAMKE MAKINI BLOG

Advertise Here

Friday 5 December 2014

TANZANIA MWENYEJI MKUTANO WA KINGA KIMATAIFA

SERIKALI ya Tanzania kupitia Wizara ya Fedha, Idara ya Kuondoa Umaskini inaandaa kongamano la kimataifa linalohusu kinga ya jamii litakaofanyika jijini Arusha kuanzia Disemba 15 hadi 17 mwaka huu.

Hayo yamesemwa leo jijini Dar es salaam na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Dkt. Servacius Likwelile wakati wa kikao cha wataalam wa sekta na waandishi wa habari kuhusu kongamano hilo.

Dkt. Likwelile alisema kuwa Mgeni Rasmi atakayefungua kongamano hilo anatarajiwa kuwa Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na unatarajiwa kufungwa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda.

Kongamano hilo litahusisha watunga sera, watafiti na watu wanaojihusisha moja kwa moja kwenye kubuni, kupanga na kutekeleza programu za kinga ya jamii na mifumo yake kwa kwa lengo la kubadilishana ujuzi na uzoefu.

Dkt. Likwelile alisema kuwa majadiliano katika kongamano hilo la siku tatu yatalega kuwajengea washiriki uelewa zaidi juu ya kinga ya jamii na matumizi yake kwa sera, programu na utawala pamoja na kushirikiana katika kutumia matokeo ya tafiti, masuala ya kujifunza na namna bora ya kuandaa na kutekeleza programu na mifumo inayohusu kinga ya jamii.

Malengo mengine ya kongamano hilo ni pamoja na kuainisha mambo ya msingi yanayohusu kinga ya jamii ambayo yanahitaji kuchukuliwa na kuingizwa kwenye agenda kuu ya kinga ya jamiii kwa ajili ya maendeleo ya usoni na kuandaa uwanja wa kubadilishana uzoefu na hatimaye kuwa na mikakati mizuri ya pamoja inayohusu kinga ya jamii.

Nchi zitakazoshiriki kongamano hilo linaloandaliwa na Serilkali ya Tanzania kwa kushirikiana na UNICEF, ILO, UNAIDS NA EPRI ni Kenya, Uganda, Bangladesh, Afghanistan,Msumbiji, Lesotho, Malawi, Afrika Kusini, Ghana, Ethiopia, Zambia, Sudan Kusini na mwenyeji Tanzania.

No comments:

Post a Comment