MWANAMKE MAKINI BLOG

Advertise Here

Tuesday 16 December 2014

DOSARI ZA UCHAGUZI MDOGO KUREKEBISWA DEC 21



UCHAGUZI wa Serikali za mitaa, vijiji na vitongoji uliofanyika jana nchini ulitawaliwa na dosari ambapo Mkoani Tanga katika baadhi ya maeneo yamelazimika kuahirisha zoezi la upigaji kura hadi DEC 21, 2014.

Maneneo ambao uchaguzi haukuenda sawa na aina ya viongozi ambao hawakuchagulia ni Kata ya Ngamiani Kati mitaa mitano kwa nafasi ya viti maamulu, Duda mitaa minne uchaguzi wa viti vitimaalumu maeneo yote haukufanyika, Majengo C wajumbe mchanganyiko hawakuchagulia, Pongwe kati wajumbe mchanganyiko, na Kata ya Kiomoni hawakuchagua Mwenyekiti, wajumbe na viti maalumu.

Mkurugenzi wa Jiji la Tanga, Juliana Malange amezungumza na Mwanamkemakini  juu ya sababu zilizosababisha kutofanyika uchaguzi huo kuwa ni kasoro zilizojitokeza kwenye karatasi za kupigia kura.

Aidha taarifa ya matokeo kwa maeneo walio piga kura ambapo CCM kwa nafasi ya mwenyekiti mitaa 118, CUF mitaa 60, Chadema mitaa 2, kwa nafasi ya Wajumbe mchanganyiko CCM 356, CUF 117 na Chadema 3, Vitimaalumu CCM 230, CUF 162 na Chadema 2.

“Katika uchaguzi huu kwa nafasi ya mwenyekiti CCM ilishinda kwa 65%, CUF 33% na Chadema 1%.

No comments:

Post a Comment