MWANAMKE MAKINI BLOG

Advertise Here

Saturday 27 December 2014

WAWILI WAUAWA TANGA MSIMU WA SIKU KUU



·       JESHI la Polisi Mkoani  Tanga linatoa shukrani kwa wananchi kwa kutoa ushirikiano  mzuri  wa kutoa taarifa za wahalifu na uhalifu kipindi hiki cha Krismas  na hivyo  kuwezesha wananchi kusherehekea  kwa amani na utulivu . 

Akitoa taarifa ya hali ya uhalifu kwa waandishi wa habari akiwa ofisini kwake kamanda wa jeshi la polisi mkoani hapa Frasser Kashai amesema wanawaomba wananchi kuendeleza ushikiano huo ili kuweza kuvuka salama mwaka 2014 kwa amani.

Aidha Kamanda Kashai amesema kutokana hali ya uvunjivu wa amani kuendelea kuijtokeza katika maeneo mbalimbali mkoani hapa kumekuwa matukio yaliyojitokeza baadhi ya Wilaya za mikoa .

Amesema  watu wawili wamefariki katika matukio mawili taofauti ,ambapo amesema mnamo tarehe 26 majira ya saa moja kamili asubuhi huko maeneo ya Ndekai Kata ya Baga   Tarafa ya Mgwashi Kando ya barabara ya Baga –Kwemakame Wilaya Lushoto ,Mtu aliyefahamika kwa jina la Rshidi Kilua  mwenye umri wa miaka mkazi wa Ndekai ,aligundua mwili wa Mpwa wake aitwe Hashimu  Rajabu  ukiwa na majereha kichwani .

Hata kamanda amesema mwili marehemu umefanyiwa uchunguzi na madaktari na kukabidhiwa kwa ndugu kwa ajili ya mazishi.

Amesema chanzo cha mauaji hayo kinasakiwa kuwa ni Migogoro ya ardhi  ,ambapo mpaka sasa watu wawili ambao ni Waziri Salimu umri wa miaka 35 mkazi wa Ndekai Baga  wapili ni Ramadhani Ayub umri wa miaka 40 mkazi wa Mwangoi  Baga wamekamatwa kufauati mauaji hayo kwa ajili ya mahojiano .

Katika tukio njingine kama hilo Mtun mmoja aliye fahamika kwa jina la Husein Muamed amefariki Dunia wakati alipokuawa anapata matibabu katika Hospitali ya Bombo mara baada ya kokolewa wakati alipokuwa akishambuliwa na wananchi waliojichukulia sheria mkononi kwa tuhuma za uwizi baada ya kuvunja nyumba na kuingia ndani kwa nia ya kuiba .Kamanda Kashai amesema upelelezi unaendelea kufuatia tukio hilo ili kuwabaini  waliojichukulia sheria mkonani.

Katika hatua nyingine jeshi la Polisi mkoani hapa linawashikilia  watu wapatao sita ambao ni ni Raia wa Ethiopia kwa kosa la kuingia Nchini bila kibali .

Kamanda Kashai amewataja watuhumiwa hao kuwani Gesamu Abato mwenye umri wa miaka 30,Hash Negash Grinanu umri wa miaka 20,Tsegaye Aliso umri wa miaka  21 ,Jamal Godso umri wa miaka 25 ,Alemayo Ataro umri wa miaka 22 na Erigudo Elitiro umri wa miaka 25 .

Kamanda Kashai amesema Watuhumiwa hao watafishwa mahakamani baada ya upelelezi wa awali kukamilika .

No comments:

Post a Comment