ASKARI
Mgambo wapatao 200 wameilalamikia ofisi ya Mkurugenzi wa Jiji la Tanga kwa
kutowalipa fedha zao kama malipo kwa kazi ya usimamiaji zoezi la kupiga kura.
Baadhi ya askari hao
MG 427805, MG 351976 na MG 265079 wakizungumza na Redio Huruma kwa niaba ya
wenzao walipofika ofisi za Jiji la Tanga wamesema licha ya kuelekezwa kumfuata
Mkurugenzi Juliana Malange ili awezeshe malipo hayo zaidi ya mara mbili juhudi
zao zimegonga mwamba bila kupatiwa majibu ya kina.
Mwandishi wetu
Rebecca Duwe alizungumza na Mkurugenzi kwa njia ya simu ambeye naye aliyolea
ufananuzi huu suala hilo kuwa yeye siye aliwewapangia vituo hivyo itamuwia
vigumu kuwatambua.
Ameongeza kwamba ni
vyema wakawasiliana na OCD ambaye atawasilisha majina kwane ili aweze
kukamilisha hayo malipo kwasababu fedha zipo kwa ajili ya kufanya hivyo.
Hata hivyo wenzao (waalimu) tayari walipatiwa malipo yao hata kabla ya zoezi kuanza.
No comments:
Post a Comment