MWANAMKE MAKINI BLOG

Advertise Here

Wednesday 10 December 2014

TAIFA LIKISHEREKEA 9 DISEMBA BASI MAARUFU NCHINI LASOMBELEA WAHAMIAJI KUWAINGIZA DAR

WAKATI Taifa likisherekea siku kuu ya TISA DESEMBA Gari yenye namba za usajili T.131 AZZ SCANIA mali ya kampuni ya Saibaba limekamatwa likiwa na  raia 12 wa  Ethiopia likiwasafirisha kutokea Arusha kuelekea jijini Dar es salaam.

Raia hao wamekamatwa majira ya saa 10:30 jioni maeneo ya Mbwiko Kata ya Mbwiko Tarafa ya Mombo barabara kuu ya Mombo –Segera Wilayani Korogwe.

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Tanga, Kamishna msaidizi mwandamizi wa Polisi Frasser kashai amewataja raia hao kuwa ni Kashoma Bayen umri wa miaka 24,Berchano Gamada umri wa miaka 32, Awal Jamal  umri wa miaka 23  ,Yanis Gatiso umri wa miaka 28, Metson Sipril  umri wa miaka 21,Tashona Hayalis umri wa miaka 30.

Wengine ni Adino Samiru umri wa miaka 20, Kengeny  Siyun umri wa miak 22 ,Charnes Egesa umri wa miaka 20, Abdi Bandru umri wa miaka 21, Siumanda Siumanda umri wa miaka 26 na Na Malako Abuu umri wa miaka 23.Watuhumiwa wote watakishwa mahakamani kujibu tuhuma inayowakabili.

MTOTO NAE KINAWA WA BIASHARA

Hawa walikamatwa siku za nyuma nchini
Wakati huo huo mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Ally Mbukuzi mwenye umri wa miaka 17 mkulima na mkazi wa Putini kata ya Chongoleani Wilaya ya Tanga kwa kosa la kuwaasafirisha wahamiaji haramu wapatao sita (6) ambao ni Raia wa Ethiopia.

kamanda Kashai amesema kuwa mnamo tarehe 8 Disemba mwaka huu majira ya saa saba 13:00 mchana, huko katika  kisiwa cha Jambe Kata ya Tongoni Tarafa ya Pongwe Wilaya Tanga wamekamatwa Dolec Dalalo umri wa miaka 28, Alaleus  Tesame umri wa miaka 21, Hashinavia Shamibu umri wa miaka 23, Taken Ndasalh umri wa miaka 20,Tamesgen Kisfon umri wa miaka 20, Mihon Eriamin umri wa miaka 22.

Aidha mtuhumiwa amekiri kufanya kufanya biashara hiyo ya usafirishaji wa wahamiaji haramu na atafikishwa mahakamani mara baada ya upelelezi kukamilika.

ONYO KALI
Jeshi la Polisi Mkoani Tanga linatoa onyo kali kwa watu wanaovunja Sheria ya Kuingiza wahamaiaji haramu kinyemela ndani ya nchi kinyume cha sheria. Jeshi la polisi litawafuatilia watu hao na kuhakikisha kwamba wanakamatwa pamoja  hamaiaji hao haramu ambao wanawasafirisha.

Aidha amewashaukuru wananchi kwa juhudi za kuendelea kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu na kuwapa ushirikiano juu ya uwepo wa wahamiaji haramu katika maeneo yao wanayoishi.

Pamoja na hayo aliwasisitizia wananchi kuendelea kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu katika maeneo yao wanayoishi ili kuweza kuzuia na kukabiliana na uhalifu mkoani hapa.


No comments:

Post a Comment