MWANAMKE MAKINI BLOG

Advertise Here

Friday 12 December 2014

MKUU WA MKOA TANGA AKABIDHIWA MAJUKUMU IKIWEMO USHIRIKIANO KWA WAKAZI WAKE







ALIYEKUWA Mkuu wa mkoa Tanga Chiku Gallawa ambaye kwa sasa ni Mkuu wa Mkoa Dodoma amewaomba wakazi wa mkoa wa Tanga kutoa ushirikiano mzuri na kumuunga mkono Mkuu wa Mkoa mpya ambaye ameletwa Tanga baada ya mabadiliko ya wakuu wa mikoa yaliyofanywa na Rais.

Katika Taarifa iliyotolewa mjini Dodoma jioni ya Jumatano, Novemba 5, 2014 na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue ilitoa maelekezo ya Mkuu Magalula Saidi aliyekuwa Mkoa Katavi kuja Tanga.

Alizungumza hayo wakati wa makabidhiano ya majukumu ya kazi baina yake na mkuu huyo mbele ya viongozi wa ngazi mbalimbali wa serikali ya Mkoa na waandishi wa habari katika ukumbi wa Mikutano wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga.

Kwa upande wake Mkuu wa sasa wa Mkoa wa Tanga Magalula saidi amewasihi wananchi kuendeleza kazi iliyoachwa na Galawa kwa mustakabali wa maendeleo ya wana Tanga.



No comments:

Post a Comment