MWANAMKE MAKINI BLOG

Advertise Here

Tuesday 16 December 2014

KITUO CHA AFYA PONGWE KIMEPOKEA TUZO YA BIMOC


WIZARA ya afya na Ustawi wa Jamii imetoa tunzo ya BIMOC kwa Kituo cha afya cha Pongwe pamoja na vyeti maalum vya daraja la kwanza. 


Hatua hii imekuja baada ya kuridhika na  huduma bora  ya dharura kwa wanawake wajawazito na watoto inayotolewa na kituo hicho.


Akifafanua maana ya BIMOC katika hafla fupi iliyofanyika kituoni hapo hii leo mganga mkuu Faisal Ally, mara baada ya kupokea tunzo hiyo amesema hiyo ni kuonyesha kuwa kituo hicho ni bora kwa huduma ya mama na mtoto


Sanjari na hayo pia Mganga huyo ameelezea uwezo mwingine walionao kituoni hapo kama vile kufanya upasuaji, kutoa dawa za usingizi, huduma ya kutoa na kuhifadhi damu salama ambayo wanategemea kuianza hivi karibuni baada ya kukamilika kwa mahitaji ya vifaa kadhaa.

Hata hivyo changamoto inayowakumba katika kutoa huduma kwa mama wajawazito ambayo hutolowa bure ameelezea kuwa ni urejeshaji wa matumizi wanayotumia kuwahudumia 

No comments:

Post a Comment