KATIKA kipindi cha miezi 11 mwaka
huu kivuko cha mto Kilombero kimeadaiwa kukusanya shilingi MIL 776,229,336
katika makusanyo yake wakati wa uvushaji watu na magari.
Hayo yalisemwa na mkuu wa kivuko cha
mto Kilombero Mhandisi Fadhil HarounMeneja kwa niaba ya Meneja wa Temesa mkoa
wa Morogoro Mhandisi Magreth Mapula kwenye kikao cha bodi ya kivuko hicho
kinachotoa huduma ya kuvusha watu na vyombo vya usafiri viendavyo na kurudi
wilayani Ulanga.
Katika ufafanuzi wake Haroun alisema
mapato yamekuwa yakiongezeka na kushuka kutokana na msimu huku akifafanua kuwa
mwezi Machi na Mei mapato yamekuwa yakishuka kutokana na hali ya mvua
kusababisha barabara kutopitika kwa urahisi watu wengi kuwa mashambani kwa
kilimo.
kwa mujibu wa meneja huyo
kunachangamoto ya mafuriko na uharibifu mkubwa wa miundombinu,magari kugonga
kivuko na kutumbukia majini,majani na nyavu kujisokota kwenye mfumo wa usukani
wa kivuko na mchanga kujaa mtoni kunakosababisha kina kupungua.
Kwa upande wao wajumbe wa bodi ya
kivuko hicho akiwemo mbunge wa jimbo la Ulanga magharibi Dk Haji Mponda
walimtaka wakala wa ufundi na umeme Temesa mkoa wa Morogoro kuharakisha ujenzi
wa vibanda vya kujikinga na mvua na jua kivukoni hapo.
Aidha walikitaka kivuuko hicho
kuongeza pato lake ili kiweze kumudu kugharimia changamoto zinazojitokeza na
kukifanya kuwa na tija katika utendaji wake.
Wazo hilo liliungwa mkono na
mwenyekiti wa kikao hicho ambaye ni mkuu wa wilaya ya Kilombero Hassan Masala
akionyesha masikitiko yake ya jinsi ambavyo mawazo ya bodi hayatekelezeki na
kukatisha tamaa bodi hiyo kwa ushauri wake.
Aidha waliutaka uongozi wa usimamizi
kivukoni hapo kutoa nafasi kwa vyombo vya usafiri vyenye abilia kupewa
kipaumbele kupita kwanza kabla ya maroli ya mizigo hasa inapotokea kunakuwa na
foleni.
No comments:
Post a Comment