
Mashindano
hayo yaliofunguliwa mwaka 1994 yamedaiwa kuwa na upendeleo mbali na rushwa
kulingana na malalamishi yaliotolewa na wananchi pamoja na washiriki.
Kwa
mujibu wa kaimu katibu mtendaji wa Baraza la Sanaa nchini Tanzania Basata ,
Godfrey Mngereza,kamati ya miss Tanzania ilikiuka kanuni na taratibu
zinazoongoza mashindano hayo.
Imedaiwa
kuwa mashindano yaliyofanyika Desemba 12, mwaka huu hayakufikia uamuzi, bali
vikao mbalimbali vilivyoendeshwa na wizara ya Habari, Utamaduni, Vijana na
Michezo kwa kushirikiana na Basata ndivyo vilivyofikia hatua hiyo ili kutoa
nafasi kwa waandaalizi kujipanga upya.
Baadhi
ya maswala yaliobainika ni kwamba baadhi ya warembo walidaiwa kutumiwa
kingono.Vilevile hakuna utaratibu wa kuwasajili warembo hao uliofuatwa kuanzia
vitongojini hadi kufikia fainali.
Mngereza
alisema baraza limegundua kuwa baadhi ya washiriki walichaguliwa kwa upendeleo
bila ya kuwa na sifa zilizohitajika
No comments:
Post a Comment