MWANAMKE MAKINI BLOG

Advertise Here

Saturday 8 November 2014

VIETEL KUVIPATIA MAWASILIANO VIJIJI ELFU 10


SERIKALI imeingia mkataba na kampuni ya simu ya Viettel kujenga mawasiliano katika vijiji elfu 10 kwa kuanzia.

Waziri wa Mawasiliano Sayansi na Teknolojia mheshimiwa MAKAME MBARAWA amesema hayo leo bungeni mjini Dodoma wakati akijibu swali la nyongeza la mbunge wa Kilwa Kaskazini.

Katika swali lake mheshimiwa MANGUNGU ametaka kujua mkakati wa serikali katika kuondokana na tatizo la mawasiliano nchini.

Mheshimiwa MBARAWA amesema kwa kuanza kampuni hiyo itaanziana vijiji  elfu 4 kuanzia sasa mpaka mwezi octoba mwakani.
Aidha kuanzia octoba mwakani hadi octoba mwaka kesho kutwa vijiji elfu 2 vitapatiwa mawasiliano ikifuatia vijiji elfu 1 mia 8 na kumalizia vijiji elfu 1 mia 2.

No comments:

Post a Comment