MWANAMKE MAKINI BLOG

Advertise Here

Wednesday 5 November 2014

YALIYOJIRI 'MJENGONI' BUNGENI DODOMA

WAZIRI wa mambo ya nchi za nje na ushirikiano wa kimataifa BERNAD MEMBE amesema serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania haijapata taarifa zozote rasmi kutoka Jamhuri ya Kenya kuhusu mgogoro wa mpaka kati ya serikali hizo mbili.

MEMBE amesema hayo leo bungeni mjini Dodoma wakati akijibu swali la mbunge baraza la wawakilishi mheshimiwa JAKU HASHIM AYOUB.

Katika swali lake mheshimiwa JAKU ametaka kujua serikali inasema nini juu ya taarifa iliyoripotiwa na vyombo vya habari kuwa kisiwa cha Pemba ni sehemu ya Kenya kufuatia mgogoro wa mpaka uliojitokeza kati ya Kenya na Somalia kuhusu vitalu vya mafuta.

Mheshimiwa MEMBE amesema kisiwa cha Pemba ni sehemu ya Jamhuri ya Muungnao wa Tanzania na kitanedelea kubakia hivyo daima na kwamba watatoa maelezo zaidi endapo tu itapokea madai hayo kutoka serikali ya Kenya.

Amesema baada ya  wizara kupata  suala hilo waliwasiliana na balozi wa Tanzania  nchini Kenya na serikali ya Kenya lakini wote walikuwa hawaelewi suala hilo limetokea wapi ila wanachofanya ni kusubiri kwa sabahu uongozi sio serikali peke yake inawezekana ilianzia kwa watu binafsi,asasi za kiraia au mashirika yasiyo ya kiserikali.

Mheshimiwa MEMBE amesema  serikali inawaomba wananchi hususan waishio katika Kisiwa cha Pemba kutokuwa na hofu yoyote juu ya maai kuwa kisiwa hicho ni sehemu ya Kenya na waendelee na shughuli za ujenzi wa Taifa kama kawaida.
MWISHO.

DODOMA
KUTOKANA na kukithiri kwa tatizo la Ujangili nchini serikali imezindua Mkakati wa Kitaifa wa Kupambana na Ujangili wa mwaka 2014 hadi 2019.

Katika mkakati huo watatoa mwongozo kwa wadau wa uhifadhi ndani ya nje ya nchi kushiriki katika mapambano dhidi ya ujangili.

Akijibu swalileo bungeni mjini Dodoma naibu waziri wa Maliasili na Utalii mheshimiwa MAHMOUD MGIMWA amesema kwacsasa wizara imechukua hatua mbalimbali za kukabiliana na tatizo hilo ikiwemo kuajiri wahifadhi wanyamapori 437 kwa ajili ya kuimarisha doria dhidi ya ujangili.

Aidha wametoa mafunzo na vitendea kazi kwa watumishi na elimu ya uhifadhi kwa jamii.

Mheshimiwa MGIMWA alikuwa akijibu swali la mbunge wa Dole mheshimiwa SYLVESTER MABUMBA aliyetaka kujua mikakati iliyochukuliwa ili kukomesha tatizo la ujangili nchini.

Katika swali la nyongeza mbunge wa Same Mashariki mheshimiwa ANNE KILANGO ametaka kujua sababu  ya serikali kuendelea kuruhusu uwindaji ilhali imekiri kuwepo kwa tatizo la ujangili.

Akijibu swali hilo mheshimiwa MGIMWA amesema suala la kuruhusu uwindaji ni masuala ya kimkataba hivyo wanangoja wapate ushauri kutoka ndai ya bunge na wao watalifanyia kazi.
MWISHO.

DODOMA
JUMLA ya miradi ya uwekezaji elfu 3,683 imesajiliwa katika kipindi cha mwaka 2010 hadi octoba 2014.

Kati ya miradi hiyo miradi elfu 1,872 sawa na asilimia  51 nimiradi ya wawekezaji wa ndani,miradi 948 sawa na asilimia 26 ni miradi ya ubia kati ya kati ya wawekezaji wa ndani na nje.

Hayo yameelezwa leo bungeni mjini Dodoma na Waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu uwezeshaji na uwekezaji mheshimiwa MARRY NAGU wakati  akijibu swali la mbunge wa viti maalum mheshimiwa RITA MLAKI.

Katika swali lake mheshimiwa RITA ametaka kujua serikali inaeleza nini bunge kwa kipindi cha miaka minne tangu kuwekwa ka wizara hiyo kuwa ni wawekezaji wangapi wameingia nchini na wamesaidia kukuza uchumi kwa kiasi gani.

Mheshimiwa NAGU amesema manufaa yanayoambatana na uwekezaji huu ni pamoja na kuongezeka kwa ajira zaidi ya laki 5,kuingizwa mitaji mikubwa,kuongezeka mapato ya serikali kupitia kodi mbalimbali zitokanazo na miradi ya uwekezaji na kupata teknolojia za kisasa.

Amesema serikali imeendelea kuhamasisha wawekezaji wote wa ndani na nje ya nchi kuwekeza hapa nchini kwa madhumuni ya kukuza uchumi wa Tanzania.
MWISHO

No comments:

Post a Comment