MWANAMKE MAKINI BLOG

Advertise Here

Wednesday 12 November 2014

UKOSEFU TAKWIMU SAHIHI KIKWAZO CHA HUDUMA BORA


BUNGE limeelezwa kuwa upungufu wa Dawa na ukosefu wa ajira hapa nchini unachangiwa kwa kiasi kikubwa na ukosefu wa takwimu.



Kauli hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uchumi Viwanda na Biashara Luhaga Mpina alipokuwa akitoa maelezo ya kamati kuhusu Muswada wa Sheria ya Takwimu ya 2013.



Mbunge Mpina  amesema kukosekana kwa takwimu kunachangia hali hiyo kutokana na kutokuwepo kwa tafiti na taarifa sahihi zinazowaongoza wanafunzi kuchagua na kusomea fani kulingana na mahitaji ya soko la ajira na vijana wengi kukosa ajira.



Amesema hivi sasa hakuna takwimu halisi za wagonjwa wanaokufa kwa kukosa matibabu na ndiyo maana maamuzi kama ya kulipa deni la MSD yamekuwa yakisuasua.



Mpina amesema uzoefu umeonyesha kuwa nchi zote ziliopiga hatua kubwa kimaendeleo zina mifumo imara ya upatikanaji wa takwimu ambazo zinasaidia kupanga mipango ya muda mfupi, wa kati na mirefu.



 Awali akisoma muswada huo Waziri wa Fedha Saada Mkuya Salum amesema madhumuni ya muswada huo ni kuipa mamlaka zaidi Ofisi ya Taifa ya Takwimu ya kutekeleza majukumu ya kitakwimu kwa uhuru na ufanisi.

No comments:

Post a Comment