MWANAMKE MAKINI BLOG

Advertise Here

Monday 10 November 2014

MAJERUHI AJALI YA TRENI MOROGORO WAKUMBUKWA



·   SERIKALI ya mkoa wa Morogoro na wadau wengine akiwemo Mwenyekiti mstaafu wa CCM mkoa wa Dar es Salaam John Guninita wamewagia misaada mbalimbali zikiwemo fedha tasilimu majeruhi wa ajali ya Basi kuigonga Treni katika hospitali ya Mt.Francis wilayani humo.

Katika misaada hiyo ofisi ya mkuu wa mkoa imetoa pole kwa majeruhi 14 kila mmoja walipata  shilingi 50,000 huku majeruhi ambae hali yake haikuwa nzuri alipewa shilingi 200,000 ili zimsaidie kuhamishiwa hospitali kuu ya rufaa Muhimbili jijini Dar es salaam.

Mbali na fedha tasilimu katika misaada iliyotolewa, misaada mingine ni pamja na maji ya kunywa, sabuni za miche na karatasi za maliwato(toilet paper) majeruhi hao.

Akikabidhi fedha hizo kwa niaba ya uongozi wa mkoa,Katibu tawala wake Eliya Ntandu alisema mkoa umesikitiswa na kutokea kwa ajali hiyo huku akiendelea kusisitiza kuwa mpango wa serikali ni kutokomeza kabisa ajali za vyombo vya moto kwa madereva kuelimishwa juu ya usalama barabarani.

Kwa upande wake Guninita alisema kuwa baada ya kupata taarifa ilibidi atoke Dar es Salaam ili kuja kuwapa pole majeruhi ukizingatia kuwa yeye ni mzaliwa wa wilaya hiyo hivyo kuguswa moja kwa moja na tukio hilo.

Guninita aliwataka wananchi wengine kjitokeza kuwasaidia majeruhi walioendelea kulazwa katika hospitali hiyo kwani wengi wao inaonekana wametoka nje ya Ifakara.

Awali Afisa uhusiano wa hospitali ya Mt.Francis Nestoly Mlagani alisema mpaka sasa chumba cha maiti umebaki mwili mmoja kati ya 11 ambapo 10 ilitambuliwa nadugu kishwa kuruhusiwa kuendelea na taratibu za mazishi.

Ajali hiyo ilitokea wiki iliyopita ilihusisha basi la kampuni ya Al Jabry lifanyalo safari zake kati ya Morogoro na Ifakara kuligonga treni la Tazara maeneo ya Kiberege na kusababisha vifo vya watu 12 huku wengine zaidi ya 30 kujeruhiwa na dereva wa basi hilo alifanikiwa kukimbia baada ya kusababisha ajali.

No comments:

Post a Comment