MWANAMKE MAKINI BLOG

Advertise Here

Thursday 13 November 2014

UVUVI HABARAMU WAWAPOTEZEA VIUNGO NA KUJERUHIWA VIBAYA

WAVUVI haramu waliokuwa wakijaribu kuvua katika kisiwa cha Karange, kata ya Tangasisi, tarafa ya Pongwe wilaya Tanga kwa kutumia baruti wamejeruhiwa na kukatika viungo vya miili yao.


Tukio hilo limetokea Novemba 12, mwaka huu majira ya saa 8:00 mchana.

Waliolipuliwa na kujeruhiwa na baruti hiyo ni Hamisi Omari Kassimu (38) mkazi wa Mwambani ambae amekatika mkono wa kulia na jicho la kulia, na Adamu Seleman Kapera (32) mkazi wa Mwambani ambae amekatika mikono yote miwili, ameumia macho yote, vidole vinne vya mguu wa kushoto na kuungua kifua.


Chombo kilichokuwa kinatumiwa kwenye uvuvi huo haramu ni Ngalawa TTA 315. Hali ya majeruhi wote ambao wamelazwa kwenye hospitali ya rufaa Bombo ni mbaya.


Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Tanga, Kamishna mwandamizi msaidizi wa Polisi SACP Frasser Kashai alisema upelelezo unaendelea kuwabaini washirika wao na mtandao mzima wa wavuvi haramu kwa hatua za kisheria.


“Tunatoa wito kwa wananchi kutoa taarifa kwenye vyombo vya usalama mara wanapowaona wavuvi wanaovua kinyume cha sheria kwa kutumia baruti kitendo ambacho kinaleta madhara kwenye rasilimali majini,” alisema Kashai na kuongeza

“Lakini pia samai hao wanaovuliwa kwa baruti wanakwa na madhara makubwa  sana kwa afya za walaji, madhara ya baruti pia ni kama mnavyoona kwa watu hao wanaotumia baruti hivyo basi taarifa zitolewe ili wahalifu washughulikiwe.

No comments:

Post a Comment