MWANAMKE MAKINI BLOG

Advertise Here

Saturday 8 November 2014

PINDA ATAKA VIJANA UVCCM KUONYESHA DHAMIRA YA DHATI

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda  akizungumza wakati alipofungua semina ya Baraza Kuu la Umoja wa Vijana wa CCM Taifa kwenye ukumbi wa  CCM White House mjini Dodoma Novemba 7, 2014. (picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
MJUMBE wa Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi CCM MIZENGO   PINDA   ameitaka  Jumuiya ya Vijana ya Chama hicho  UVCCM kuonyesha dhamira ya Kweli katika kuimarisha mshikamano na umoja walionao.

Akifungua semina ya siku tatu iliyowahusisha wajumbe wa baraza kuu la umoja huo Taifa mjini Dodoma mheshimiwa PINDA ambaye pia ni waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amesema  umoja huo ndio ngome ya CCM hivyo wakishikamana itakuwa rahisi kuwakatisha tamaa maadui.

Amesema watu  wengi wanapenda kuwaona wakifarakana  lakini wasikubali na wakatae jambo lolote lenye lengo la kudhoofisha umoja na mshikamano walionao ili waweze kujipanga mapema kwa ajili ya ushindi.

Akizungumzia kuhusu Katiba pendekezwa  PINDA amesema  vijana wanapaswa kutembea vifua mbele na wasikubali kudanganywa kwa kuwa Katiba hiyo ni bora  na imeundwa kwa mfumo shirikishi.

Amesema kazi  iliyofanyika ni nzuri na wala hawataijutia ingawa kuna baadhi ya wajumbe walitoka nje lakini kazi iliendelea na katiba pendekkezwa imepatikana.

Awali akimkaribisha mgeni rasmi mwenyekiti wa Jumuiya hiyo Taifa SADIFA JUMA HAMISI amesema  UVCCM ipo imara na wataenda kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa wakiwa wamoja na kuleta ushindi.

Mada malimbali zinatarajiwa kuwasilishwa katika semina hiyo ikiwemo ushindi katika uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu na mada kuhusiana na katiba Pendekezwa.

No comments:

Post a Comment