MWANAMKE MAKINI BLOG

Advertise Here

Saturday 8 November 2014

MALAWI HAIITAMBUI TANZANIA KAMA MMILIKI ZIWA NYASA



  • Yakwamisha maandalizi mradi usimamizi rasilimali za asili
 
MAANDALIZI ya mradi  wa kuboresha usimamizi wa rasilimali za asili za bonde la Ziwa Nyasa yamekwama baada ya nchi ya Malawi kutoiambua Tanzania kama mojawapo ya nchi zinazomiliki ziwa hilo.


Akijibu swali bungeni  mjini Dodoma waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi dr TITUS KAMANI amesema ziwa hilo la Nyasa linamilikiwa na nchi tatu ambazo ni Tanzania,Malawi na Msumbiji.

Amesema nchi hizo kwa pamoja katika mwaka wa 2010 zilikuwa katika maandalizi ya mradi huo ambayo yalikwama.

Amesema juhudi za kutafuta suluhu kuhusu mgogoro huo zinaendelea katika ngazi za kimataifa.

Hata hivyo dr KAMANI amesema serikali inajenga karakana ya kutengeneza boti za uvuvi eneo la Mbaba Bay ili kuwawezesha wavuvi kupata boti imara kwa urahisi,kufanya uvuvi wenye tija na hivyo kujiongezea kipato.

Dr KAMANI alikuwa akijibu swali la mbunge wa viti maalum mheshimiwa CYNTHIA HILDA NGOYE aliyetaka kujua miradi inayotekelezwa na serikali kwa ajili ya kuwasaidia wavuvi katika vijiji vya kata za Ngonga,Matema,Mwaya,Kijunjumela,Katumba na Songwe wilaya ya Kyela mkoani Mbeya.

No comments:

Post a Comment