MWANAMKE MAKINI BLOG

Advertise Here

Friday 28 November 2014

KUSAHAULIKA WIMBO WA UKIMWI, NI KUZOELEKA MASIKIONI AMA TUNA MENGI MAKUBWA YAKUIMBA ZAIDI

Siku ya Ukimwi Duniani inaadhimishwa kila tarehe 1 Desemba kama siku maalumu ya kupanua ufahamu kuhusu maafa yanayoletwa na ugonjwa wa Ukimwi.
Desemba mosi ilichaguliwa kuwa siku ya Ukimwi kutokana na tarehe hiyo kuwa ndiyo siku ambayo virusi cha Ukimwi kilitambulika rasmi mwaka 1981. Toka mwaka 1981 hadi 2007 watu zaidi ya milioni 25 wameshafariki kutokana na Ukimwi. Mwaka 2007 peke yake walifariki milioni 2, kati yao watoto 270,000.
Siku hiyo ilichaguliwa rasmi mwaka 1988 wakati wa Mkutano wa Dunia wa Mawaziri wa Afya Kuhusu Mpango wa Kuzuia Ukimwi. Kuanzia hapo siku hiyo imekuwa ikikumbukwa rasmi na serikali, mashirika yasiyo ya kiserikali, na wanaharakati.
Toka mwaka 1988 hadi 2004, Siku ya Ukimwi Duniani ilikuwa ikiratibiwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Masuala ya Ukimwi (UNAIDS). Mwaka 2005 UNAIDS ililipa shirika lisilo la kiserikali la Kampeni ya Ukimwi Duniani (the World AIDS Campaign) wajibu wa kuratibu siku hiyo.
Kila mwaka siku hiyo hufanyika kwa ujumbe maalumu. Ujumbe wa mwaka 2005 hadi mwaka 2010 ulikuwa, "Zuia Ukimwi: Timiza Ahadi".

Uratibu wa Mwitikio wa Taifa dhidi ya janga la UKIMWI Print
Mkakati wa Pili wa Taifa wa Kudhibiti UKIMWI (2008 – 2012)
Uratibu wa MwitikioMkakati wa Pili wa Taifa wa Kudhibiti UKIMWI (NMSF) unahusu kipindi cha kuanzia mwaka 2008 hadi 2012. Unaendeleza mafanikio na uwezo wa Mwitikio wa Taifa wa Mapambano dhidi ya UKIMWI katika kipindi cha miaka mitano kilichopita (kuanzia mwaka 2003 hadi 2007) na kupendekeza hatua za kuchukuliwa ikiwemo mikakati ya kukabili vikwazo na matatizo vilivyopita. NMSF huu unaelekeza mikabala, afua na shughuli vitakavyofanywa na watendaji wote nchini. Mkakati huu umetayarishwa baada ya mapitio makubwa na mchakato wa ushauriano chini ya maelekezo ya wataalamu wa Kitaifa na Kimataifa.

Mpaka sasa UKIMWI ni tishio kubwa la maendeleo ya Taifa na umetangazwa kuwa ni janga la Taifa. Athari yake inasababisha kuenea kwa mateso miongoni mwa watu binafsi, familia na jamii nchini kote. Hata hivyo kuna dalili za matumaini. Kulingana na taarifa na takwimu za hivi karibu ushamiri wa VVU hauendelei na hata kufikia kupungua kidogo katika sehemu nyingi za Tanzania. Juhudi za kinga na upatikanaji wa matibabu yanayofaa vimepunguza athari ya UKIMWI miongoni mwa watu walioambukizwa. Hata hivyo, bado kuna Watanzania zaidi ya milioni moja walioambukizwa VVU na maambukizo mapya yanatokea nchini kila siku. Ukubwa wa janga hili na jumla ya athari zake katika kipindi cha miaka ishirini iliyopita bado vinaleta changamoto kubwa nchini, changamoto ambazo zinaweza kukabiliwa kwa njia ya kuongeza juhudi shirikishi.

Mafanikio na changamoto
Miaka mitano iliyopita ya Mwitikio wa Taifa wa Mapambano Dhidi ya UKIMWI iliongozwa na Mkakati wa Kwanza wa Taifa wa Kudhibiti UKIMWI (2003-2007). Katika miaka hii, kumepatikana mafanikio makubwa yaliyochangia kuimarisha juhudi za Kitaifa.

Miongoni mwa mafanikio makubwa katika maeneo manne yaliyodhamiriwa ni haya yafuatayo:

Mazingira yanayowezesha (masuala mtambuko):
Wizara, Idara na Wakala na Mamlaka za Serikali za Mitaa zimeanzisha kiasi fulani cha afua kwa ajili ya waajiriwa wao na sekta zao; VVU na UKIMWI vimefungamanishwa katika Mpango wa Muda mrefu wa Kupunguza Umaskini (MKUKUTA); TACAIDS imeweza kuwa mratibu mkuu wa mwitikio wa Taifa wa Kudhibiti UKIMWI; Waratibu wa UKIMWI wameteuliwa katika Wizara, na Idara, Wakala na Mamlaka za Serikali za Mitaa zote na Kamati za Kudhibiti UKIMWI ziliundwa; Kamati Shirikishi za Kudhibiti UKIMWI zilianzishwa katika Wilaya zote na katika baadhi ya Kata na Vijiji na mafunzo yalitolewa kwa wanakamati; Wakala za Uwezeshaji za Mkoa zilianzishwa katika Mikoa yote na zimetoa msaada mkubwa kwa Wilaya na Jamii;

Cheo cha Naibu Waziri wa Maafa na VVU na UKIMWI kilianzishwa katika Ofisi ya Waziri Mkuu; Umoja wa Wabunge wa Mapambano dhidi ya UKIMWI Tanzania ulianzishwa; Vyama vya Kiraia vingi vimekuwa vikijishughulisha na VVU na hivyo kutoa uelewa wa kutosha nchini vikiwemo vikundi vingi zaidi vya WAVIU; Fedha kwa ajili ya shughuli za VVU na UKIMWI ziliongezwa zaidi kutoka Serikali na Wahisani na fedha nyingi zaidi zilifikia jamii; Kulikuwa na upanuzi zaidi wa mfumo wa kufuatilia maambukizo ya VVU; Utafiti wa mara kwa mara ulifanyika kuhusu VVU na mwenendo (ukiwemo VVU na UKIMWI katika Utafiti wa Hali ya Afya ya Watanzania)na Utafiti wa Kiashirio cha VVU Tanzania; Kulikuwa na uunganishaji wa utoaji taarifa kuhusu VVU na UKIMWI katika mfumo wa afya; na Kulikuwa na uendelezaji na uanzishwaji wa mfumo wa ufuatiliaji kwa ajili ya shughuli zisizokuwa za afya (TOMSHA).

Kinga:
Matibabu ya maambukizo kwa ngono yaliongezeka katika hospitali na vituo vya afya vyote na asilimia 60 ya zahanati; Kumekuwa na ongezeko kubwa la upatikanaji wa kondomu za wanaume nchini (kutoka milioni 50 hadi milioni 150); Vituo vya Unasihi na Upimaji wa Hiari vimeongezeka zaidi ya mara tatu; Uzuiaji wa Uambukizo wa VVU kutoka kwa Mama kwenda kwa Mtoto umeongezeka hadi kwenye asilimia 12 ya hospitali na vituo vya afya; Kutokana na utafiti mbalimbali, kulikuwa na uthibitisho kwamba vijana wameanza kubadili mienendo yao ya ngono (ongezeko la kuchelewesha shughuli za ngono, wapenzi wachache wa ngono n.k.) na programu za uendelezaji wa afya shuleni zilipanuliwa, na; Sekta binafsi na zisizo rasmi zimejihusisha zaidi na mapambano dhidi ya UKIMWI kwa kutoa programu za kinga na matunzo kwa waajiriwa na jamii kwa ujumla.

Matunzo na Matibabu:
Mpango maalumu wa Tiba ya Kuongeza Kinga ya Mwili umetekelezwa na zaidi ya WAVIU 70,000 wamepewa matibabu hadi mwisho wa 2006, na Miradi ya matunzo nyumbani imepanuliwa hasa na vyama vya kiraia.

Upunguzaji Athari:
Misaada iliongezeka kwa mayatima, watoto wanaoishi katika mazingira magumu na vikundi vingine vinavyoishi katika mazingira magumu; na Kulikuwa na uhusishaji wa WAVIU katika Mwitikio wa Taifa hasa Uraghibishi na upunguzaji wa unyanyapaa na ubaguzi.

Hata hivyo, katika mwitikio wa jumla, bado kuna changamoto nyingi zinazohitaji kushughulikiwa kwa miaka ijayo. Miongoni mwa changamoto hizo ni: Upungufu wa utashi wa kisiasa katika ngazi ya kati na ya chini pamoja na uwajibikaji wa mwitikio wa VVU;

Programu chache na hafifu za VVU katika Wizara, Idara, Wakala na Mamlaka ya Serikali za Mitaa hasa katika ngazi za mikoa, wilaya na kufikia jamii; Chombo cha uratibu cha Kitaifa chenye majukumu mengi (TACAIDS); Kutotambuliwa na kutotumika kwa kanuni ya “Dhana Tatu” katika ngazi ya Serikali kuu na Wilaya. Uhusishaji mdogo wa vyama vya Kiraia na WAVIU hasa katika mipango na utekelezaji wa mwitikio wa VVU kwenye ngazi ya Wilaya na jamii; Ucheleweshaji wa mara kwa mara na matatizo katika kutoa fedha kwa wakati kwa Wilaya na Jamii; Uwezo mdogo katika Mamlaka za Serikali za Mitaa wa kuandaa na kutekeleza mipango kabambe ya VVU na UKIMWI; Unyanyapaa na ubaguzi bado ni vya kiwango cha juu katika jamii; Juhudi za kinga hazikushughulikia kiasi cha kutosha masuala ya afya ya ujinsia na uzazi na mara nyingi hazikutekelezwa; Bado kumekuwa na matatizo ya matumizi sahihi na ya mara kwa mara ya kondomu na upatikanaji mdogo katika jamii nyingi za vijijini; Uenezaji mdogo wa juhudi za kinga katika maeneo ya vijijini, na; Upatikanaji wa Tiba ya kuongeza Kinga ya Mwili ulikuwa katika vituo vya mijini tu.


KABLA YA SAA 24 KUPITA UNAHAKI YA KUJUA HAYA JUU YA ESCROW

WASIRA AFUNGUKA YAKE ASEMA HADI WATU KUBEBA FEDHA KWENYE LUMBESA HAKUNA NCHI HAPA!
Wasira: CAG sio mara ya kwanza kuchunguza na kuleta taarifa bungeni, na PAC nao hii ni kazi yao kuchunguza na kuleta Bungeni
Wasira: Jambo la pili ni wajibu sasa wa Bunge hili kutazama ripoti hizi na kuzifanyia kazi.
Wasira: Kama kuna mtu anataka kuwa Rais na mbinu zake ni kuondoa wengine huyo hafai kabisa kuwa Rais wa Tanzania
Wasira: Sisi bunge hili lazima tunangalie maslahi ya Watanzania, hatuwezi kutumiwa na mtu.
Wasira: Afadhali kuwa maskini mwenye heshima kuliko tajiri anayetukanwa
Wasira: Tutakuwa Bunge la ajabu kama maneno haya yameandikwa na vyombo hivi vya Bunge halafu sisi tukalifumbia macho.
Wasira: Nchi ambayo unaenda na sandarusi, mabox kubeba hela, hapa hatuna nchi, inabidi TAKUKURU watutajie ni kina nani hawa
Wasira: TAKUKURU iwachambue watu wote bila kujali vyama au nini ili tuwapeleke kwenye sheria
Mwandosya: Suala hili linatuondolea sifa kama nchi, linatuondolea heshima kama taifa, kimataifa na mbele za wananchi

HALIMA MDEE NA MNYIKA WAFUNGUKA YA KWAO JUU YA ESCROW
Bunge limekutana tena sasa na msemaji wa kwanza aliyekaribishwa ni @jjmnyika
jjmnyika : Utata uliokuwepo juu ya kifo cha Mh. William Mgimwa aliyekuwa Waziri wa fedha, wengine wakausisha kifo kile na ulaji wa fedha hizi za Escrow
Mnyika: Muhongo lazima awajibike kwa kujizuru na lazima awajibike kwa wananchi
Mnyika: Linapokuja suala la uwajibikaji kwa Mawaziri wa kawaida linaonekana sawa ila inapokuwa Waziri Mkuu mnamkingia kifua
Mnyika: Kama mtakumbatia hili suala tutachukua hatua za kupiga kura juu ya kukosa imani na Waziri Mkuu:
halimamdee : Mwanasheria Mkuu unatakiwa utupishe uende Tarime ukapumzike
halimamdee : Tukirogwa tukianza kudai kodi manaake ni kwamba serikali tumehararisha wizi huu
halimamdee : Mahakama kuu ya Tanzania haikuwa na mamlaka yoyote kushughulikia fedha za ‪#‎TegetaEscrow‬

KIGWANGALLAH ASEMA KUWA HAJAWAHI ONA PROF MUONGO KAMA WAZIRI MUHONGO
hkigwangalla : Wana CCM wenzangu itakuwa jambo la ajabu sana kama tutajiunga kuwa genge la kutetea uovu.
Ukisoma ripoti ya CAG kwa umakini hizi dhana zote za Mh. Muhongo ni uongo mtupu.
Kigwangallah: Muhongo ni mzoefu wa kusema uongo, mimi binafsi sijawahi kuona Prof. MUONGO kama huyu Prof Muhongo.
Kigwangalla: Ripoti zote alizotoa huko nyuma ni uongo hata jana amesimama na kusema uongo
hkigwangalla: Toka lini CAG akaenda kukagua fedha za mtu binafsi
Toka lini fedha za mtu binafsi zikakaa benki kuu?

Thursday 27 November 2014

A BETTER WORLD YASAIDIA UJENZI VYOO BORA MOMBO



·     TAASISI ya A BETTER WORLD ya Canada imesaidia ujenzi wa matundu ya vyoo 16 yaliyogharimu Mil. 16.5 kwa shule ya msingi Misajini iliyopo Mombo wilayani Korogwe.

Taarifa hiyo imetolewa na Mwalimu wa Shule hiyo Elizabeth Mathew kwa Muasisi wa Shirika hilo nchini Eric Rajahamba kwenye uzinduzi wa mradi huo unaolenga kuboresha afya za wanafunzi.

Mwalimu Mathew amesema amesema kufadhiliwa kwa mradi huo ni matokeo mazuri ya mahusiano Mtanzania Azidi Kaoneka na taasisi hiyo ambae pia aliwai kuwaunganisha na wafadhili waliofanikisha mradi wa maji na upanuz wa madarasa.

KWA HILI LA ESCROW AWAMU YA TATU IMEVUNJA REKODI

RIPOTI ya Kamati ya bunge ya Hesabu za Serikali imewataja baadhi ya vigogo wanaohusika na kashfa ya IPTL Nchini Tanzania akiwemo Waziri Mkuu na kuwataka kuwajibika kisiasa na kisheria.
 
Sakata hiyo ya IPTL inahusihswa na upotevu wa mamilioni ya fedha na kwa muda mrefu umezusha mjadala mzito katika bunge.

Katika ripoti hiyo iliyowasilishwa na mwenyekiti wa kamati hiyo Zitto Kabwe na makamu mwenyekiti Deo Filikunjombe, imethibitisha kuwepo mazingira ya udanganyifu na ufisadi katika mchakato wa malipo yaliyofanyika na kueleza kuwa upotevu huo wa fedha ungeweza kudhibitiwa kama kungekuwa na uwajibikaji wa kutosha kwa baadhi ya viongozi.

Kamati hiyo imewataja viongozi wengine wanaotakiwa kuwajibika kutokana na kashfa hiyo kuwa ni mwanasheria, Waziri wa nishati na Madini, Naibu Waziri wa Nishati pamoja na viongozi wengine wa bodi.

Ripoti hiyo ilitokana na ukaguzi uliofanywa na Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ambayo ilianika ukiukwaji mkubwa wa taratibu wakati wa uchotaji wa fedha hizo pia mahojiano na mkurugenzi mkuu wa Takukuru na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

Waziri Pinda anadaiwa kuwa alijua kuwapo kwa ufisadi huo na matamshi yake kuwa fedha hizo hazikuwa mali ya umma, wakati Mwanasheria Mkuu Jaji Frederick Werema ameonekana kutoishauri vizuri Serikali na pia kuagiza fedha hizo zitolewe kwenye akaunti hiyo.

Waziri Sospeter Muhongo amelaumiwa kwa kukosa kuchukua hatua wakati akijua kuwapo kwa sakata hilo, huku naibu wake, Stephen Masele akitiwa hatiani kwa kulidanganya Bunge.

Kashfa nyingine zilizowahi chukua uzito mkubwa katika bunge nchini na kusababisha viongozi kuwajibika wakiwemo Waziri Mkuu ni pamoja na kashafa ya Richmond, EPA na sasa hii ya ESCROW ambayo kwa mara nyingine kamati hiyo imeonyesha wazi mapendekezo yake ya kutaka kuwajibika kwa waziri mkuu, Mawaziri na viongozi wengine.

AJALI YAUA 13 TANGA, WAMO INSPECTER WA POLISI NA SISTER WA ANGLICAN



WATU 13 wamethibitishwa kufa na wengine 19 kujeruhi baada ya basi dogo aina ya Coaster la kampuni ya ''Thende Sheki'' yenye namba za usajili T 410 BJD kugongana uso kwa uso na lori la mizigo Scania namba T 605 ABJ katika eneo la Mkanyageni lililopo wilayani muheza.
 
Katika ajali hiyo, iliyotokea majira ya saa 1:30 asubuhi ya leo Coaster lilikuwa likitoka mkoani Tanga kuelekea wilayani Lushoto likiwa limepakia abiria 27.
 
Baadhi ya majeruhi wa ajali hiyo wamesema dereva mwenye lori alikuwa akiyumba njia nzima kabla ya kukutana uso kwa uso na gari dogo la abiria aina ya Coaster hatua waliyodaiwa kuwa dereva huyoo alikuwa amepitiwa na usingizi.

Kaimu kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Tanga Juma Ndaki amethibitisha ajali hiyo na kuwataja madereva kuwa ni wa Coaster Bakari Mussa amevunjika mkono wa kulia na wa Scania Banjamini Abeli ameumia kichwa na miguu.

Waliofariki kwenye ajali hiyo ni Sister Hellena wa Kanisa la Mt Augustino Anglican Chumbageni, Salumu Hussein (30), Muddy Mohamedi (35), Ahmed Shemdoe (48), Julius Manyama (60), Zawad Juma (35), Frida Benjamini ambae hakufahamika umri mara moja.

Wengine ni Inspecta wa Polisi wilaya ya Muheza Antony Masanya, Kadiri Alfani (29), na wengine majina yao bado hayajatambuliwa.

Wednesday 26 November 2014

WAHITIMU WA KIDATO CHA SITA MWAKA 2014 NA KIDATO CHA NNE MWAKA 2013 WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA JESHI LA POLISI BAADA YA USAILI KUKAMILIKA

Maelekezo Muhimu.
  1. Wahitimu wa kidato cha sita mwaka 2014, kidato cha nne mwaka 2013 na JKT Mafinga, Mlale, Ruvu, Mgambo, Bulombola, Kanembwa, Itende, Nachingwea, Mbweni, Maramba, Chita, Makutupola, Mtabila, Msange, Mgulani, Oljoro, Rwankoma na Kimbiji wamechaguliwa kujiunga na mafunzo ya awali ya Jeshi la Polisi.
  2. Wahitimu hawa waliochaguliwa wanatakiwa kuripoti tarehe 28/11/2014 kwa Makamanda wa Polisi wa Mikoa kama ilivyooneshwa kwenye jedwali hapa chini ili waandaliwe usafiri wa kuwapeleka Shule ya Polisi Tanzania tarehe 30/11/2014.
  3. Zoezi la usajili litaanza shuleni hapo tarehe 01/12/2014 hadi tarehe 15/12/2014. Atakaefika kuanzia tarehe 16/12/2014 hatapokelewa.
  4. Atakaeamua kuripoti kwa Kamanda wa Polisi ambako hakupangiwa atalazimika kujigharimia usafiri hadi Shule ya Polisi Tanzania mjini Moshi.
  5. Vijana hawa watalazimika kufika shuleni wakiwa na mahitaji yafuatayo:
    1. Vyeti vyao vyote vya masomo( original Academic Certificates/Result slip pamoja na Leaving certificates) kidato cha Nne/Sita, Vyeti vya kuzaliwa (Original Birth certificates). Hati ya kiapo cha kuzaliwa haitakubalika.
    2. Mashuka mawili rangi ya Bluu Bahari (light blue)
    3. Chandarua chenye upana futi tatu
    4. Nguo za michezo(Track suit nyeusi,Tshirt blue na Raba)
    5. Pasi ya Mkaa
    6. Ndoo moja
    7. Pesa za kulipia bima ya afya kiasi cha shilingi elfu hamsini na mia nne tu (50,400/=).
    8. Pesa kidogo ya kujikimu.
  6. Kwa mujibu wa kanuni za shule ya Polisi ni marufuku kufika shuleni na simu ya mkononi. Atakayepatikana na simu atafukuzwa shuleni hapo. Shule itaelekeza na kusaidia kufanya mawasiliano.
  7. Angalia orodha ifuatayo:Orodha ya walioitwa kwenye-usaili

Tuesday 25 November 2014

DC PANGANI AWAJIA JUU WAKWAMISHA UJENZI WA MAABARA



·   MKUU wa wilaya ya Pangani Hafsa Mtasiwa amesema kuwa hatamvumilia mtu yeyote atakaeonekana kukataa au kushawishi jamii kutoshiriki katika uchangiaji wa ujenzi maabara badala yake atamchukulia hatua kali za kisheria.

Mtasiwa ametoa kauli hiyo wakati akipokea msaada wa bati 200 yenye thamani ya shilingi milioni nne kutoka kwa Muko wa hiaadhi ya jamii PSPF ikiwa ni mchango wao wa kuunga zoezi la ujenzi wa maabara linaloendelea nchini kote.

Amesema kuwa katika wilaya hiyo kuna baadhi ya shule bado ujenzi unasuasua kutoka na wananchi kukosa ushawishi wa kuchangia ujenzi huo.

Nae Afisa mfawidhi wa mfuko wa hifadhi ya jamii PSPF Salome Makala alisema kuwa wameamua kuchangia ujenzi huo ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za serikali katika kuhamasisha elimu.

WANAWAKE WATAKIWA KUJITOKEZA KUGOMBEA UONGOZI




WANAWAKE wameshauriwa kutokuogopa kujitokeza kugombea nafasi mbalimbali za uongozi kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa.

Ushauri huo umetolewa na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mheshimiwa Ummy Mwalimu wakati akifungua baraza la Umoja wa Wanawake wa Chama cha Mapinduzi UWT wilaya ya Mkinga.

Amewata kutokuogopa kujitokeza kuchukuwa fomu kwa ajili ya kugombea nafasi mbalimbali za uongozi kwenye ngazi za vijiji,vitongoji na kata.

 Pia aliongeza kuwa ni wajibu wao kuhakikisha CCM inachukuwa nafasi zote za ugombea wa vijiji na kata kwenye wilaya hiyo.

Katika hatua nyingine Naibu waziri aliweza kutoa kadi kwa wanachama 200 wapya waliotoka kwenye vyama vya upinzani.