MWANAMKE MAKINI BLOG

Advertise Here

Sunday 26 October 2014

YALIYOMPELEKA WAZIRI MKUU MIZENGO PINDA POLAND


WAZIRI MKUU Mizengo Pinda atatuma wataalamu wa sekta ya kilimo kufuatilia suala la mahitaji ya trekta ili kuziba pengo la mahitaji yake nchini Tanzania.

Alisema lengo la Serikali la kuanzisha sera ya Kilimo Kwanza lilikuwa ni kuwasaidia wakulima kupata ruzuku ya pembejeo, mbegu bora, na dawa za mifugo ili waweze kuongeza ushalishaji.

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akipata maelezo kutoka  kwa mshauri wa uchumi nchini Polland Bw, Aleksandr Zincman (kulia) wakati alipotembelea  kiwanda cha kutengeneza  maghala ya kuhifadhia nafaka (silos), mashine za kukausha nafaka na mashine za kusafisha nafaka cha Chojnow nchini Polland akiwa katika ziara ya kikazi nchini humo Oktoba 24, 2014. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
“Kutokana na mkopo wa Serikali ya India, tulipata matrekta 1,846 ambayo hayakuchukua muda kuisha. Sasa hivi tunatafuta wabia wengine wa kutupatia zana za kisasa za kilimo kwa sababu matunda yake mazuri tumeyaona, tunataka kilimo cha Mtanzania,” alisema.

Jana asubuhi (Ijumaa, Oktoba 24, 2014), Waziri Mkuu alitembelea kampuni ya Farmers inayotengeneza vipuri pamoja na matrekta ya kulimia na kuvuna yenye ukubwa wa Horse Power 80 na 72 ambayo alielezwa kwamba yanavumilia hali ya udongo mgumu wa Afrika.

Waziri Mkuu Mizengo Pinda akikagua matrekta yanayotengenezwa katika kiwanda cha  ROL- BRAT  kilichopo Warsaw, Polland akiwa katika ziara ya kikazi nchini humo Oktoba 24, 2014. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Akitoa taarifa kwa Waziri Mkuu, Mtendaji Mkuu wa kampuni ya Farmer, Bw. ZDZISLAW ZUKIEWICZ alisema vifaa vinavyotengenezwa na kampuni hiyo vina waranti ya miaka saba na vinaweza kuhimili udongo wa miamba na mawe wa ardhi ya Tanzania.

Kampuni hiyo inatengeneza matrekta, mashine za kuvuna mazao shambani (combined harvester), mashine za kukata nyasi za malisho ya mifugo pamoja na vipuri vyake. Alisema bei ya trekta ni wastani wa Euro 22,000 na wako tayari kuleta vifaa hivyo Tanzania kama watapewa oda.

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na wajumbe wa Chama cha Wafanyabiashara cha Polland  jijini Warsaw akiwa katika ziara ya kikazi nchini humo Oktoba 24, 2014. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Waziri Mkuu amemaliza ziara yake ya siku tatu nchini Poland jana mchana ambapo asubuhi alikutana na Watanzania waishio Poland na baadaye kufanya vikao na baadhi ya wafanyabiashara wa jiji la Warsaw.

No comments:

Post a Comment