MWANAMKE MAKINI BLOG

Advertise Here

Sunday 26 October 2014

CHUO KIKUU HURIA TANGA CHAFUNGUA MWAKA MPYA WA MASOMO 2014




WAKAZI wa mjii wa Tanga wameshauriwa kujitokeza kwa wingi kwenda kujisomea katika Chuo Kikuu Huria (OUT) tawi la Tanga ili kujipatia elimu bora itakayo wasaidia kukuza ufanisi wa shughuli zao za kila siku.

Hayo yamesemwa katika ufunguzi wa mwaka wa masomo 2014 na mkuu wa Mkoa wa Tanga Luteni mstaafu Chiku Galawa wakati wa hotuba yake ambaye ndiye aliye kuwa mgeni  rasmi  katika ufunguzi  huo.

Sanjari na hayo amewataka pia waajiri kuwapa nafasi  wafanyakazi wao pindi  wanapo  taka  kwenda kujisomea  kwani kwakufanya hivyo kutawezesha   kuwasaidia   kujipatia  elimu  endelevu itakayo weza kuwasaidia  kwa mambo mbali mbali

Sambamba  na hayo  Mkurugenzi  chuoni  hapo Rahma Muhamedi  amewataka wanachuo  wajue  kutumia Computer  ili kuweza kujisomea masomo mbali mbali pamoja na kufanya mitihani inayo tolewa kwa njia ya mitandao.

No comments:

Post a Comment