MWANAMKE MAKINI BLOG

Advertise Here

Monday 13 October 2014

WAKRISTO WATAKIWA KUWA CHANJO CHA AMANI YA FAMILIA


WAKRISTU nchini wametakiwa kuzifanya familia zao kuwa ni chanzo cha upendo, furaha na uimara katika imani ili kupunguza maovu ndani ya jamii na taifa kwa ujumla.

Rai hiyo imetolewa na Padre Prochecy Kasongo Paroko wa Kanisa Kuu la Mtakatifu Patriki Jimbo Katoliki la Morogoro ambaye ni katibu wa tume ya familia wa baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania kwenye adhimisho la ibada ya misa takatifu ya jumapili.

Katika ibada hiyo iliyoadhimisha kanisa kuu la mtakatifu Anthony wa Padua jimbo la Tanga Kasongo alisema kila mmoja ndani ya familia anatakiwa kuishi kikamilifu na kujitambua nafasi yake ili kuwa na maisha ya kumpendeza mungu.

Hata hivyo padre Kasongo hakusita kuwakumbusha wakrtistu kutambua kila mwanadamu ameubwa kwa makusudi ya Mungu hivyo basi ni vyema kutambuwa uthamani wapekee machoni pake, kwa tutimize wajibu wa  kumcha yeye muumbaji wetu.

No comments:

Post a Comment