MWANAMKE MAKINI BLOG

Advertise Here

Thursday 23 October 2014

TANZANIA YAJIVUTA NAFASI 5 JUU, LISTI YA FIFA UBORA DUNIANI

LEO FIFA imetoa Listi ya Ubora Duniani na Mabingwa wa Dunia Germany bado wako Nambari Wani wakifuatiwa na Argentina na Colombia wakati Tanzania imepanda Nafasi 5 na kukamata Nafasi ya 110.

Mabingwa wa zamani wa Dunia, Spain, wamezidi kuporomoka na sasa wapo Nafasi ya baada kushuka Nafasi 2 huku Brazil wakibakia pale pale Nafasi ya 6.
Nao England wanazidi kushuka na safari hii wameshuka Nafasi 2 na kushika Nafasi ya 20.

Timu ya juu kabisa kwa Afrika ni Algeria ambayo iko nafasi ya 15 baada kupanda Nafasi 5. Listi nyingine itatolewa hapo Tarehe 27 Novemba 2014.


20 BORA:
1        Germany      [Ipo pale pale]
2        Argentina    [Pale pale]
3        Colombia     [Pale pale]
4        Belgium       [Imepanda Nafasi 1]         
5        Netherlands[Imeshuka Nafasi 1]
6        Brazil          [Pale pale]
7        France         [imepanda Nafasi 2]
8        Uruguay      [Imeshuka Nafasi 1]
9        Portugal      [imepanda Nafasi 2]         
10      Spain          [imeshuka Nafasi 2]
11      Italy  [Imepanda Nafasi 2]
12      Switzerland  [Imeshuka Nafasi 2]
13      Chile  [Imeshuka Nafasi 1]
14      Croatia       [Imepanda Nafasi 5]         
15      Algeria        [Imepanda Nafasi 5]         
16      Costa Rica  [Imeshuka Nafasi 1]
17      Mexico        [Imeshuka Nafasi 1]
18      Greece       [Imeshuka Nafasi 4] 
19      Ukraine      [Imepanda Nafasi 5]
20      England     [Imeshuka Nafasi 2]

ILIPO TANZANIA:
106    Belarus                 
107    Sudan                   
108    Palestine     
109    Malawi        
110    Tanzania [Imepanda Nafasi 5]              
111    Ethiopia                
112    Cuba 
113    Namibia      
113    Jamaica                
115    St. Kitts and Nevis           
116    Kenya  

No comments:

Post a Comment