MWANAMKE MAKINI BLOG

Advertise Here

Monday 13 October 2014

VITUO 600 KUTOLEA CHANJO SURUA-RUBELLA TANGA

ZAIDI ya vituo 600 vya kutolea chanjo vitatumika Mkoani hapa kutolea chanjo ya Surua-Rubella kwa watoto wenye umri wa miezi 9 hadi miaka 15, kampeni itakayoanza tarehe 18 hadi 24 octoba, 2014 kwenye vituo vyote vya kutolea huduma za afya, shuleni na vile vitakavyoandaliwa na halmashauri.

Mkuu wa Mkoa wa Tanga Kapteni (Mstaafu) Chiku Ghallawa akifungua mkutano wa Kamati ya Huduma ya Afya ya Msingi uliolenga maandalizi ya Kampeni ya chanjo ya Surua-Rubella


Akizungumza kwenye Mkutano wa kamati ya huduma ya Afya ya msingi, Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Kapteni (mstaafu) Chiku Gallawa aliwataka viongozi wa dini wejitolee  kuwahamasisha wananchi katika  maeneo mbalimbali ili waweze kuitikia wito wa kushiriki  katika zoezi hilo muhimu kwa maendeleo ya taifa.

“Kila mtu kwenye nafasi yake aweke jitihada stahiki kufanikisha zoezi hili, tuwaelimishe jamii kuachana na imani potofu juu ya uvumi kwamba chanjo hizi zinamadhara, serikali ni makini haiwezi kuruhusu chanjo yenye madhara kwa wananchi wake,” alisema Gallawa.
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga Asha Mahita akizungumza kwenye Mkutano huo, muda mfupi kabla ya kumkaribisha Mkuu wa Mkoa Gallaawa
Wajumbe wa Kamati ya Huduma ya Afya ya Msingi Mkoa wa Tanga, wakifuatilia kwa makini mkutano huo.

Wajumbe wa Kamati ya Huduma ya Afya ya Msingi Mkoa wa Tanga, wakifuatilia kwa makini mkutano huo (wawili mbele) pamoja na baadhi ya waandishi wa Habari Mkoa wa Tanga.


Serikali chini ya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii inaendesha zoezi hilo kwa kushirikiana na Shirika la Afya Duniani (WHO) na  Shirika la kuhudumia Watoto Duniani (UNICEF) kwa lengo la kudhibiti magonjwa yayoweza kuzuilika ikiwa ni utekelezaji wa mpango wa kuboresha afya za wananchi. 

Nae Mganga mkuu wa Mkoa wa Tanga Asha Mahita, alisema pamoja na chanjo hii, watoto wenye umri wa miezi 6 hadi 59  watapatiwa matone ya Vitamini A huku dawa za minyoo zikitolewa kwa wale walio na umri kunzia mwaka 1 hadi miezi 59 na utoaji wa chanjo ya dawa za Matende na Mabusha litawahusisha wananchi wote walio na umri wa kuanzia miaka 5 hadi 100.

Awali mwakilishi wa Wizara ya Afya nchini Dkt Ibrahim Maduhu alisema chanjo hiyo ina umuhimu mkubwa kwa wanawake wenye umri wa kuzaa na wajawazito kwa kuwa itawakinga na athari ya kuzaliwa na ngozi yenye vipele, homa, tatizo la mtoto wa jicho, mtindio wa ubongo, ulemavu na tatizo la Moyo.

Kampeni ya chanjo hii kitaifa itazinduliwa siku hiyo ya Oktoba 18 ambapo zaidi ya asilimia 46 watanzania wanatarajiwa kunufaika ambapo kaulimbiu ya mwaka huu ni “Linda, Okoa maisha ya Mtoto-kamilisha chanjo”.

No comments:

Post a Comment