MWANAMKE MAKINI BLOG

Advertise Here

Friday 24 October 2014

KAMPENI YA WANAWAKE NA UCHUMI KUNUFAISHA WAJASIRIAMALI 300 MKOANI TANGA



KAMPUNI ya Angels Moment ya Jiiji Dar es salaam kuwapatia wanawake wapatao 300 wajasiriamali wa Mkoa wa Tanga elimu ya biashara katika kampeni ya MWANAMKE NA UCHUMI ili kuwajengea uwezo na uelewa utakao ibua hisia chanya kutambua fusa walizonazo kiuchumi.

Mafunzo hayo ya siku mbili yatagusa masuala ya Ujasiriamali, Utunzaji wa hesabu za Biashara, uwekaji wa Akiba, umuhimu wa rasimali Ardhi na masuala ya Afya bora.

 

Akizungumza kwenye mkutano a waandishi wa habari wa mkoa wa Tanga, Mkurugenzi wa Kampeni ya Wanawake na Uchumi kutoka kampuni ya Angels Moment, Mahada Erick amesema kuna fursa nyingi za utajiri kwa wajasiriamali ambazo wengi wameshindwa kuzitambua kutokana na uelewa mdogo walionao.


Mkuu wa wilaya ya Tanga Halima Dendego (mwenye nguo ya manjano), pamoja na Mkurugenzi wa Kampeni ya Wanawake na Uchumi kutoka kampuni ya Angels Moment, Mahada Erick.




Mkuu wa wilaya ya Tanga Halima Dendego, kushoto kwake ni Mkurugenzi wa Kampeni ya Wanawake na Uchumi kutoka kampuni ya Angels Moment, Mahada Erick, Donald Lembeli afisa mwandamizi Uendeshaji kutoka NSSF, upande wa kulia ni Baraka Mtoi Afisa Masoko Mkoa wa Tanga, GEPF na Gastory Meneja Mkuu wa Naivera Complex kutoka.




"wanawake wengi wakiwemo wa Mkoa huu wa Tanga, kama mnavyojua wamekuwa wahanga wa kukumbwa na madeni, na kukatiza biashara na ujasiriamali kwa sababu ya kukosa elimu au kukumbwa na changamoto mbalimbali,” alisema Erick na kuongeza.



Moja ya changamoto ni kufanya manunuzi yasiyo yalazima mfano magauni mengi, dhahabu huku wakishindwa kuelewa kuwa hivyo vitu ni mtaji na vinaweza kununulia mashamba na rasilimali nyingine za kuendeleza biashara.



Nae Mkuu wa Wilaya ya Tanga amesema kuwa semina hiyo itakayofanyika Naivera Complex Novemba 5 na 6 mwaka 2014, imekuja kwa wakati muafaka kwa wajasiriamali kujikuza kibiashara na kiuchumi.




 Kwa upande wao afisa mwandamizi Uendeshaji kutoka shirika la hifadhi ya jamii NSSF Donald Lembeli na Baraka Mtoi Afisa Masoko mfuko wa GEPF Mkoa wa Tanga, wamesema kupitia mpango maalumu wa kuwakomboa wanawake wtakuwa bega kwa bega kuendelea kuwahamasisha ili waweze kukopesheka fedha za mashirika kupitia kwenye saccos na kujiwekea akiba.


Kwa upande wao afisa mwandamizi Uendeshaji kutoka shirika la hifadhi ya jamii NSSF Donald Lembeli na Baraka Mtoi Afisa Masoko mfuko wa GEPF Mkoa wa Tanga, wamesema kupitia mpango maalumu wa kuwakomboa wanawake wtakuwa bega kwa bega kuendelea kuwahamasisha ili waweze kukopesheka fedha za mashirika kupitia kwenye saccos na kujiwekea akiba.



Angels Moment wa kushirikiana na Wizara ya Maendeleo ya Jamii jinsia na watoto pamoja na taasisi ya WAMA imeshanufaisha wanawake 1600. 

Kampeni hii pmoja na Mkoa wa Tanga inatarajia kuwafikia wanawake wa vikundi vya ujasiriamali, SACCOS, VICOBA na makundi mengine ya kijamii kwenye mikoa ya Pwani, Lindi, Ddodoma, Kigoma, na Ruvuma.




Waandishi wa Habari wanaume (waliosimama) katika picha ya pamoja.


Waandishi wa Habari wanawake (waliosimama) nao hawakuwa nyuma.

No comments:

Post a Comment