MWANAMKE MAKINI BLOG

Advertise Here

Tuesday 21 October 2014

NOTI BANDIA ZAMPONZA KIJANA


Kamanda wa Jeshi la Polisi Tanga, Freser Kashai

KIJANA mmoja, mkazi wa Makorora mkoani hapa amepatikana na noti 11 bandia za shilingi elfu 10 za kitanzania zenye thamani Tshs.110,000 na noti nne za dola 100 bandia za kimarekani .

Khalid Ramadhani kijana wa miaka 28 amepatwa na noti hizo Octoba 19, 2014 mnamo majira ya saa 10 za jioni kwa saa za Afrika mashariki.

Kijana huyo ameelezwa kuwa ni mkazi wa Mikanjuni kata ya Mabawa Tarafa ya Ngamiani kati Wilaya ya Tanga mjini Mkoa wa Tanga.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Tanga, Kamishna mwandamizi Msaidizi wa Polisi, SACP Freser Kashai amesema mtuhumiwa huyo amekiri kufanya biashara hiyo ya uuzaji wa noti bandia.

Ramadhani atafikishwa mahakamani wakati wowote kujibu tuhuma za biashara hiyo haramu baada ya upelelezi kukamilika.

No comments:

Post a Comment