MWANAMKE MAKINI BLOG

Advertise Here

Thursday 23 October 2014

ELIMU YA CHANJO IONGEZWE KWA WATANZANIA



SERIKALI imeshauriwa kuendelea kutoa Elimu kwa wanachi wote juu ya umuhimu wa chanjo ya  magonjwa ya Surua na Rubella inayo endelea kutolewa hapa  nchini kutokana wananchi wengi waliojitokeza kuwa na uelewa mdogo kuhusu chanjo hiyo.

Hayo yamebainishwa na Mwalimu Asha Mbwana wa shule ya msingi Chuda ambaye niongoni mingoni mwa watoa   huduma  kwa wananchi katika hospitali ya Ngamiani jijini Tanga wakati akizungumza mwandishi wa redio huruma  hospitalini hapo.

Aidha mwalimu huyo amesema kuwa uelewa wa wananchi juu ya zoezi la chanjo inayotolewa hivi sasa imekuwa ni ndogo hivyo ameishauri serikali iendelee kutoa ushikiano na cvyombo vya habari ili kuhakikisha wananchi wote wanaelewa umuhimu wa huduma hiyo.

Naye afisa Afya wa hospitali ya Ngamiani Alfa Allan Ameishukuru serikali kwa jitihada za uhamasishaji wa kuhudhuria chanjo kwani wanapokea takribani  watoto 500 kwa siku  huku watu wazima  ni   1000 wanaofika hospitalini hapo.  

Sambamba na hayo ametoa wito kwa wananchi wote kupenda kupima afya zao mara kwa mara ili kujua maendeleo ya afya zao lakini pia  kuwa  wakweli pale wanapohisi kuwa na  dalli zozote  wa magonjwa ili wqapatiwa matibabu kwa haraka na kwa wakati.

No comments:

Post a Comment