MWANAMKE MAKINI BLOG

Advertise Here

Wednesday 29 October 2014

TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA TANGA KWA VYOMBO VYA HABARI



KUJINYONGA
MTU mmoja aliyefahamika kwa jina la Biasin Isaa 35 mkulima na mkazi wa Mdolwa Bali Kutu amefariki dunia baada ya kujinyonga kwenye mti wa maembe karibu na nyumbani kwake kwa kutumia Khanga.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo Naibu wa Kamanda wa polisi mkoani hapa Juma Ndaki amesema tukio hilo limetokea mnamo tarehe 27 octoba mwaka huu  majira ya saa 5 huko Mdolwa kijiji cha uuga Bazo Kata ya uuga na Tarafa ya soni Wilaya ya Lushoto .

Aidha Naibu wa kamanda Ndaki amesema chanzo cha kifo cha marehemu huyo ni msongo wa mawazo  na mwili wa marehemu umefanyiwa uchunguzi na daktari na kukabidiwa kwa ajili ya mazishi.

KUCHOMWA
MTU mmoja aliyefahamika kwa jina la Francis Mwendi Mkaburu 70 mkulima na mkazi wa kijiji cha Nyamaleni amefariki dunia baada ya kuchomwa moto akiwa ndani ya nyumba yake na watu wasiojulikana.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo Naibu wa Kamanda wa polisi mkoani hapa Juma Ndaki amesema tukio hilo limetokea mnamo tarehe 28 octoba mwaka huu majira ya 1 huko kijiji cha Nyamwela kata ya Pagwi na Tarafa ya Kwekivu Wilaya ya Kilindi.

Sambamba na hayo naibu wa kamanda Ndaki amesema chanzo cha mauaji hayo ni kuhusiana na imani za kishirikina.

Pia Naibu wa kamanda Ndaki amesema msako mkali unaendelea katika kubaini watuhumiwa waliohusika na tukio hilo.

No comments:

Post a Comment