MWANAMKE MAKINI BLOG

Advertise Here

Wednesday 4 June 2014

MIKAKATI YA TANZANIA NA MIUNDOMBINU

 



WAZIRI MKUU Mizengo Pinda  amesema Tanzania ni miongoni mwa nchi za kwanza katika Jumuiya ya Afrika Mashariki kuingia kwenye ubia na sekta binafsi katika mradi mkubwa wa usafirishaji abiria.

 Ametoa kauli hiyo leo mchana  wakati akifungua Mkutano wa siku mbili wa  Majadiliano yenye lengo la kuutangaza mradi wa mabasi yaendayo kasi kwenye ukumbi wa Mlimani City Pinfa amesema kutèkelezwa kwa mradi huo kutatoa fursa za ubunifu utakaowezesha kupatikana suluhisho la usafiri mijini hasa inayokua kwa kasi barani Afrika.

 Amesema ni matumaini ya Serikali kwamba wadau kutoka sekta binafsi ambao ni wazawa na wa kutoka nje ya nchi watashiriki kwenye mradi huu ili uweze kuboresha matumizi ya kadi ambayo mtu hatatakiwa kulipia fedha taslimu akiwa ndani ya basi bali kutumia kadi anayoilipia kabla ya kuingia ndani ya basi husika.

Mapema, akiwakaribisha wajumbe wa mkutano huo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Hawa Ghasia amesema Serikali imedhamiria kuhakikisha kuwa mradi huo unafanikiwa  na kushukuru Benki ya Dunia ambayo imetoa dola za Marekani milioni 200 kwa ajili ya kufadhili mradi huo.

Mkutano huo unawashirikisha wadau mbalimbali wakiwemo wa ndani na wa nje wanaotarajiwa kutoa huduma za mabasi makubwa na madogo, utoaji tiketi, ulinzi, usafi na huduma za maduka.
 

No comments:

Post a Comment