MWANAMKE MAKINI BLOG

Advertise Here

Thursday 5 June 2014

DODOMA KINARA WATOTO WA MITAANI




MKOA wa Dodoma umetajwa kuongoza  kitaifa  kwa kuwa na tatizola  watoto wa mitaani kwa kiwango cha asilimia 13.3.

Takwimu hizo zimeainishwa  mjini Dodoma  na katibu tawala msaidizi wa mkoa wa Dodoma ndugu Deogratius Yinza katika kikao cha wadau cha kujadili tatizo la watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi na watoto wa mitaani.

Amesema mkoa wa Dodoma una ongezeko kubwa la watoto hao ambapo  wilaya zinazoongoza kwa mkoa wa Dodoma ni wilaya ya Bahi ikifuatiwa na wilaya ya Chamwino na Mpwapwa.

Amesema takwimu za kimkoa za mwaka jana kuanzia januari hadi disemba  zinaonyesha kuwa Dodoma ina watoto wa mitaani 49,829 ambapo kati ya hao wavulana nio 25,860 na wasichana ni 23,968.

Ametaja sababu kubwa ya ongezeko hiloni sababu ya kibinadamu ambapo familia nyingi zimekosa muelekeo na kusababisha kutelekeza familia zao,kutumikishwa na ukatili wa kijinsia.

Yinza ametoa wito kwa wadau kutambua changamoto zilizopo katika tatizo hilo ili waweze kupambana kupunguza tatizo hilo na kusisitiza wadau kuzitambua sheria zinazomlinda mtoto na kuzitekeleza kulingana na mikataba ya kisheria iliyopo.

Ametaka kukomeshwa kwa mila zilizopitwa na wakati ambazo zinawakandamiza watoto na kuwabagua kulingana na jinsia zao na kuwafuatilia wazazi na walezi kama wanatoa haki na stahili kwa watoto wao ili watakaokaidi wachukuliwe hatua.

No comments:

Post a Comment