MWANAMKE MAKINI BLOG

Advertise Here

Monday 9 June 2014

MAJAMBAZI YATOKOMEA NA T.SH 1,378,600 ZA MFANYABIASHARA



WATU wanaodhaniwa kuwa majambazi wapatao nane wakiwa na silaha mbalimbali za jadi wamemvamia na kumopora fedha mfanyabiashara mpakani mwa Kenya na Tanzania.
Mfanyabiashara huyo ambae ni mkazi katika kijiji cha Jasini wilayani Mkinga alitambuliwa kwa jina la Mohamed Tembo 30. Watu sita wanashikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoani Tanga kuhusiana na Tukio hilo.

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Tanga Costantine Masawe amethibitisha tukio hilo na kusema kuwa Tembo alivamiwa usiku wa kuamkia leo majira ya saa 7:30 usiku ambapo pia walifanikiwa kutokomea na fedha taslimu sh 978,600/=.

Katika tukio jingine la June 8 mwaka huu majira ya Saa 2:30 usiku huko Pingoni Mjohoroni Pande Mkoani hapa, Sixmudi Kakurumu 62 mkazi wa Pande amevamiwa na watu wasiojulikana na kumjeruhiwa sehemu mbalimbali za mwili wake kisha kumpora sh 400,000/=.

Watu hao wapatao nane waliokuwana na silaha za jadi ikiwemo mapanga na marungu walipora pia vitu mbalimbali vya dukani ambavyo thamani yake haikuweza kufahamika mara moja

Kamanda Masawe amesema wanaendelea kufanya juhudi za kuwapata watuhumiwa hao wakati Kakurumu akiendelea kuuguza majeraha katika hospitali ya mkoa wa Tanga Bombo.

No comments:

Post a Comment