MWANAMKE MAKINI BLOG

Advertise Here

Thursday 5 June 2014

AJALI MSAFARA WA MWENGE IRINGA

MSAFARA wa mbio za Mwenge wa Uhuru mkoani Singida umeingia dosari ukiwa katika siku yake ya kwanza baada ya kutokea ajali inayohusisha magari matatu, yakiwemo mawili ya polisi, kwenye kijiji cha Kirumbi, mpakani mwa mkoa wa Tabora na Singida.
Kwa mujibu wa mashuhuda kutoka eneo la ajali, ajali hiyo imetokea muda wa saa 6.30 mchana ambapo inadaiwa gari STK 3288 lililokuwa limewabeba wahudumu wa afya  kuliparamia kwa nyuma gari la polisi namba PT 1980.

Gari hilo lenye usajili PT 1980 lililazimika kusimama ghafla kutokana na gari lingine la polisi  namba PT 2010 lililokuwa mbele yake kupata pancha na kusimama katikati ya barabara.

Mashuhuda hao wamedai kuwa mara baada ya kutokea kwa ajali hiyo, askari polisi watatu waliokuwemo kwenye gari namba PT 1980 waliumia sehemu mbalimbali za miili yao, ikiwemo kuvunjika  mikono na miguu, na  mmoja wao hali yake ni  mahututi.

Askari wote watatu wamepelekwa hospitali ya Rufaa ya St, Gasper Itigi kwa matibabu zaidi.

No comments:

Post a Comment