MWANAMKE MAKINI BLOG

Advertise Here

Wednesday 4 June 2014

DAKTARI HOSPITALI KATOLIKI MATATANI KWA UDANGANYIFU



 
Jengo la kanisa katoliki Jimbo la Tanga (Picha na Maktaba)
JESHI  la polisi mkoani  humu  linamshikilia  Daktari wakituo cha afya cha tumaini Richard  Kafuru mwenye umri wa miaka 60  mkazi wa Majengo kwa tuhuma za kukutwa na nyaraka hewa za bima ya afya ofisini kwake.

Akitoa ufafanuzi juu  ya   tuhuma hizo kaimu kamanda wa polisi mkoani hapa    Juma Ndaki  amesema  Daktari huyo amekamatwa kupitia taarifa zilizotolewa na muuguzi na msimamizi wa kituo hicho Sir.Flora Mushi mwenye umri wa miaka  48 mkazi wa chumba geni  jijini humu.

Amesema muuguzi huyo aligundua majina mbalimbali ya hewa ya wagonjwa waliotibiwa mwezi wa januari mwaka huu visivyo halali kwa kutumia bima ya afya.

Aidha kaimu kamanda huyo amesema nyaraka hizo ni Kadi 15 zenye namba na majina tofauti, Hati za kuchukulia dawa kituoni hapo na maduka ya dawa yaliyoidhinishwa na bima ya afya, ambapo alitumia majina ya madaktari wenzake katika fomu hizo.

Hata hivyo amesema mtuhumiwa huyo alikutwa na madaftari sita ya wagonjwa ambayo ni kinyume na taratibu ya bima ya afya wanapoingia mkataba wa vituo vya afya au maduka ya kutolea madawa.

Sanjari na hayo Ndaki amesema uchunguzi wa awali umebaini  hasara ya   shilingi milioni 45 katika kituo hicho ambapo mtuhumiwa huyo ambaye ni   daktari    anashikiliwa na jeshi la polisi kwa hatua zaidi.

Akizungumza kwaniaba ya msimamizi wa kituo hicho Sir Alfonsina Sangawe  amesema  ni kwel daktari huyo amefanya kosa la kudhalilisha kituo pamoja na kanisa, hivyo wamemfukuza kazi na hatakuwa mtumishi tena kituoni hapo.

No comments:

Post a Comment