MWANAMKE MAKINI BLOG

Advertise Here

Thursday 5 June 2014

WANWAKE WATAKIWA KUTOBWETEKA



WANAWAKE Mkoani Morogoro wametakiwa kutokata tamaa katika shughuli za kiuchumi ili kuondokana na utegemezi pia ombaomba kwa wanaume zao na jamii.

 Ushauri huo umetolewa na mwenyekiti wa umojawa wanawake mkoa wa morogoro Mariam Kyamani kwenye sherehe ya miaka 10 ya kikundi cha kijamii cha Upendo women group  kilichopo kata na mtaa wa Tubuyu manispa ya Morogoro.

Kyamani ambaye pia ni diwani wa kata ya Kingolwila amesema dhana ya mwanamke kuendelea kuwa tegemezi imepitwa na wakati badala yake wanatakiwa kujishugulisha kulimngana na flsa walizonazo.

Katika risala ya kikundi hicho pamoja na mambo mengine iliomba mashirika na taasisi mbalimbali kuendelea kusaidia vikudi vya kijamii kwa ajili ya kuleta mabadiliko ya kinamama ya kiuchumi.

Naye katibu wa mbunge Morogoro mjini Morisi Masala aliyemwakilisha mbunge huyo aliwataka wanawake kusitahimili mikikmiki inayojitokeza katika vikundi na kuzitatua zao  ili kuimalisha vikundi hivyo. 

Amesema katika vikundi hivyo wajitahidi kuboresha elimu  kwa kuwapeleka watoto shule kwa kipato kidogo wanacho kipata.

Upendo women group kilianznzishwa mwaka 2005 kikiwa na wanachama 6 kwa lengo la kusaidiana katika shida na raha .

Kikundi hicho ambacho sasa kinawanachama 30 mpaka sasa kimeshatoa huduma mbalimbali za kijamii kwa watoto yatima na wazee wasiojiweza katika mtaa wa Tubuyu katani humo.

Kwa mjibu wa mwenyekiti wa kikundi hicho martha Tanika kikundi hicho kinajiendesha kwa kutumia ada zao wenyewe na miradi mbalimbali ya  kukodisha maturubai ,zabuni za kupika chakula cha sherehe na shughuli za kupamba katika sherehe.

No comments:

Post a Comment