MWANAMKE MAKINI BLOG

Advertise Here

Saturday 14 June 2014

UKATILI HADI LIN!I: KICHANGA ATUPWA NDANI YA TUNDU LA CHOO

KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida mwanamke mmoja anaesadikiwa kuwa mkaazi wa mji wa Pongwe jijini Tanga ambaye hakuweza kutambulika mara moja amejifungua mtoto mwenye jinsia ya kike kisha muda mfupi baadae kumtupa chooni.

Tukio hilo la kinyama na la kusikitisha limetokea usiku wa Juni 12 ambapo watu wengi walikuwa makini kwenye luninga zao kufuatilia mchezo wa kwanza wa michuano ya kombe la Dunia unaoendelea nchini Brazil.
Muonekano wa Choo hicho kwa nje
 
Wakizungumza mwanamkemakini.blogspot.com wakazi wa eneo hilo wamesema kuwa wamefanya jitihada za kumnusuru mtoto huyo licha ya kuwa hadi sasa mtuhumiwa hajatambulikana.

Hili ndilo tundu alimo tupwa kichanga hicho
Nae Balozi wa mtaa wa Misufini Mohamed Mbogo amekiri kupokea taarifa hizo alizozipata asubuhi ya majira ya saa 1:30 Juni 13 kutoka kwa Polisi Jamii.
Majirani wakiwa kwenye nyumba alipotupwa kichanga chooni

Mtoto huyo kwa sasa anaendelea kupata matibabu kwenye hospitali ya Mkoa wa Tanga Bombo na Polisi wanaendelea na uchunguzi ili kumbaini aliefanya ukatili huo.

No comments:

Post a Comment