MWANAMKE MAKINI BLOG

Advertise Here

Thursday 5 June 2014

UMOJA WA BODABODA NI DAWA HAYA?


UMOJA wa waendesha pikipiki maarufu kama bodaboda na waendeshaji wa bajaji mjini hapa (UWAKIBATA) wametakiwa kuendelea kuitii sheria za usalama barabrani ili kuepukana na ajali zinazotoke mara kwa mara.



Hayo ameyasema Kamanda wa kikosi cha usalama barabarani Mkoani Tanga, Abdi Isango kwenye mkutano wa uchaguzi wa viongozi mbalimbali wa chama hicho uliofanyika katika ukumbi wa Polisi, (police mess) mjini hapa.


Aidha Isango ameeleza kuwa chaguzi huo ni ili madereva hao wapate kutambua umoja wao ambao viongozi wake watakuwa na jukumu la kusaidiana na Jeshi hilo kuangalia usalama wa madereva hao.


Hata hivyo amesema chama kwa kushirikiana na jeshi la polisi watahakikisha kuwa waendesha bodaboda wanazitii sheria zilizowekwa na viongozi wao na wale ambao watahusika na uvunjaji wa sheria hizo watachukuliwa hatua.


Kwa upande wake mwenyekiti ambaye amechaguliwa kwenye uchaguzi huo Daudi Bilali amesema anatarajia juona madereva hao wanaendelea kuitii sheria ili kuisaidi serikali majukumu.


Sambamba na hayo amewomba waendesha bodaboda kutoa elimu kwa abiria juu ya uvaaji wa kofia ngumu za element ili kuondoa wasiwasi wa kupatwa na maradhi.

No comments:

Post a Comment