MWANAMKE MAKINI BLOG

Advertise Here

Monday 9 June 2014

MFANYABIASHARA AJIUA KWA KUJIPIGA RISASI TANGA

 
MFANYABISHARA mmoja mkazi wa Michungwani wilaya ya Muheza mkoani Tanga, Ally Rajabu Makufya 72, amejiua kwa kujipiga risasi ya shingo kwa kutumia bunduki.

Marehemu ambaye pia ni mmiliki wa baa mbili wilayani Muheza amejiua June 8 majira ya saa 3; 30 asubuhi akiwa chumbani kwake akitumia bunduki yake anayoimiliki kihalali.

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Tanga amethibitisha tukio hilo.
Wakati huohuo June nane majira ya saa 8:20 mchana watu wa wawili Jofrey Daniel (20) mkazi wa kwanjeka na Musa Hamisi miaka 44 mkazi wa Mtambwe Mkoani hapa wamekamatwa wakiwa na bunduki Raifo yenye namba 2703520 iliyowahi kuripotiwa na Musa Hamisi 44 kwamba imeibiwa.

Watu hao wanaosadikiwa kuwa ni majambazi wamekamatwa maeneo ya Ngomeni barabra kuu ya Muheza -Tanga pia wakiwa na risasi mbili za bunduki hiyo, ganda moja la risasi, panga moja, kisukimoja na bisi bisi mbili.

No comments:

Post a Comment