MWANAMKE MAKINI BLOG

Advertise Here

Wednesday 7 January 2015

WAWIILI MBARONI MAUAJI YA WANAHABARI UFARANSA



POLISI wa Ufaransa wametoa majina na picha ya washukiwa wawili waliohusika na shambulio katika ofisi za jarida la vibonzo nchini humo.

Polisi wamemtaja Said Kouachi na kaka yake Cherif wanaweza kuwa watu hatari na wenye silaha.

Cherif Kouachi aliwahi pia na kuhusika na kupeleka wapiganaji wenye msimamo mkali wa kidini nchini Iraq.

Vyombo vya Habari vya Ufaransa vimesema mtu wa tatu ambaye amegunduliwa pia kama ni mshukiwa Hamyd Mourad mwenye umri wa miaka 18 alijisalimisha polisi baada ya kuona jila lake katika mitandao ya kijamii.

Baadhi ya rafiki zake walisema katika mitandao hiyo kwamba alikuwa shule wakati shambulio hilo katika ofisi za jarida la vibonzo la Charlie Hebdo likitokea, ambako watu 12 waliuawa.

Uchunguzi mkali bado unaendelea kuwasaka watu hao wenye silaha.
Awali jarida hilo lilipandisha hasira kwa waislamu baada ya kuchapisha kibonzo walichodai kuwa ni Mtume Muhamad SAW.

Jana polisi nchini Ufaransa walisema kuwa wanaume waliokuwa wamejifunika nyuso wamewaua takriban watu 12 kwenye ofisi za gazeti moja la vibonzo la Charlie Hebdo.

Watu wengine watano wameripotiwa kujeruhiwa vibaya.Gazeti hilo lililo mjini Paris limekuwa likilengwa na wanamgambo wa kiislamu siku za nyuma.

Tukio hilo lilitokea mapema asubuhi wakati watu waliokuwa na silaha walipoingia katika ofisi za gazeti hilo na kuanza kufyatua risasi na kisha wakatoroka wakitumia gari.

Rais wa ufaransa Francois Hollande amelaani shambulizi hilo akisema kuwa nchi hiyo imepatwa na mshangao mkubwa.

Inaarifiwa washambulizi walisikika kwa sauti ya juu wakisema ''tumelipiza kisasi kw aniaba ya Mtume Muhammad.'

Rais Francois Hollande alisema hapana shaka kwamba shambulizi hilo ni la kigaidi

Waandishi wanne wa jarida hilo la vibonzo, akiwemo mhariri mkuu Stephane Charbonnier walikuwa miongoni mwa waliouawa pamoja na maafisa wengine wawili.

Vyombo vya habari vimewataja wachoraji wengine watatu waliouawa wakiwemo, Cabu, Tignous na Wolinski. Duru zinasema shambulizi hilo lilifanyika wakati wa mkutano wa kila mwezi wa uhariri wa jarida hilo.

No comments:

Post a Comment