MWANAMKE MAKINI BLOG

Advertise Here

Thursday 29 January 2015

KILINDI KUANZA KUNUFAIKA NA UMEME WA KINYESI




NA MASHAKA MUHANDO, KILINDI
BAADHI ya wananchi wa wilaya ya Kilindi mkoani Tanga wataanza kunufaika na nishati ya umeme utokanao na kinyesi cha ng’ombe hatua ambayo itawawezesha kumudu gharama za maisha njia ambayo pia imeelezwa kuwa itasaidia kupunguza vitendo vya uharibifu wa mazingira kwa kutojihusiaha na ukataji miti ovyo ili kupata kuni na mkaa.

Juma Kilo ambaye ni mwezeshaji kupitia shirika la NCRF alimweleza mwandishi wa habari hizi juzi kuwa tayari amefanikiwa kuwapatia elimu baadhi ya wananchi wa wilaya ya Kilindi na wamehamasika kutumia nishati hiyo ambapo sasa utaratibu unaandaliwa ili kuweza kufungiwa mitambo inayohusika.

Kilo ambaye ni mkazi wa kata ya Mnyuzi wilayani Korogwe ambaye naye anatumia nishati hiyo katika familia yake mara baada ya kupatiwa elimu kabla ya kuwa mhamsishaji kutokea wilayani Korogwe alivitaja vijiji ambavyo watu wake wameelimishwa ni Songe, Kwinji, Kilindi, Mafisa na Kilindi yenyewe.

Kuhusu gharama za mitambo ya umeme wa kutumia kinyesi Kilo alisema kuwa kwa mtambo mdogo inatakia kiasi cha Tsh 700,000/= huku ul e mkubwa ukichukua Tsh 1.2 mil ambapo malighafi zinazotumika katika ujenzi ni saruji, mawe na mchanga huku akisistiza kuwa uendeshaji wake hauna gharama.

Mbali na kuzungumzia suala la uenezaji wa nishati hiyo ya umeme wa kinyesi, Kilo alisema tayari wamegundua mbolea bora ya yenye tija isiyo haribu ardhi inayotokana na kinyesi hicho ambapo taratibu mbalimbali zinafanyika katika kuizalisha na hivyo kuleta mazao yenye tija na ubora kwa wakulima.

Alisema kuwa mbolea hiyo haina kemikali ambazo huharibu mazingira ila ni rafiki wa mazingira na hivyo jamii kuwa na uhakika wa kuwa na mazingira yaliyo salama katika kipindi chote cha maisha yao ambapo aliwashauri wananchi kuzitembelea ofisi za NCRF Korogwe ili kupatiwa ushauri utakaowasaidia.

Mhamasishaji huyo aliendelea kusema kwamba tayari soko la mbolea hiyo inayozalishwa kwa kinyesi cha ng’ombe ni kubwa na bei yake ni yenye faida kubwa huku akiyataja naadhi ya maeneo ambayo mradi wa NCRF umefika kuwa ni Pongwe nje kidogo ya jiji la Tanga, Muheza, Usangi, Lushoto na Mkinga.

No comments:

Post a Comment