MWANAMKE MAKINI BLOG

Advertise Here

Thursday 29 January 2015

WANASHERIA WATAKIWA KUTUNGA SHERIA NDOGO VIJIJINI



BAADA ya kubainika sheria ndogo za vijiji ‘by law’ kushindwa kuwawajibisha wanaokiuka taratibu wanasheria wa halmashauri za wilaya wametakiwa kushirikiana na serikali kutengeneza na kuboresha sheria zilizopo.

Hayo yamebainishwa na washiriki wa mafunzo ya siku tatu ya ufuatiliaji na uwajibikaji wa jamii kwenye sekta ya afya kwa washiriki 90 iliyojumuisha viongozi wa vijiji, kata, madiwani na wananchi wa kawaida.

Semina hiyo iliyoanza juzi inaendeshwa na shirika la Hale Development Organization HADEO.

Walisema hali hiyo imejitokeza baada ya wanasheria wa halmashauri kutokuwa tayari kufika waliko wananchi hao na kushindwa kushirikiana nao katika kutengeneza sheria zilizopo ama kuziboresha kwa manufaa ya jamii.

Awali Diwani wa kata ya Magoma Hadija Mshahara alisema iwapo watendaji watasimamia sheria kikamilifu hali ya unyonge itaweza kuwaondokea.

Kauli hiyo ya diwani huyo ilichangiwa na watendaji na wananchi wakielezea mapungufu ya kisheria yaliyopo hivi sasa wakisema zimeshindwa kufanya kazi katika eneo la Mahakama ambapo mwezeshaji wa semiha hiyo aliwakumbusha kwamba bado hilo liko kwenye uwezo wao na halmashauri.

Katika semina hiyo ya mafunzo iliyofanyika kwenye ukumbi wa chuo cha ualimu TTC wilayani Korogwe wafadhili wa mafunzo hayo walikuwa ni shirika la The Foundation for civil society ambapo shughuli ya mafunzo iliendeshwa na shirika la Hale Development Organization HADEO la wilayani Korogwe.

No comments:

Post a Comment