MWANAMKE MAKINI BLOG

Advertise Here

Thursday 29 January 2015

MAKUSANYO YA NDANI KOROGWE MJI YANUFAISHA VIKUNDI 106



NA EVELYN BALOZI, TANGA
HALMASHAURI ya mji wa Korogwe imefanikiwa kuwainua wanawake na vijana kupitia mikopo ya fedha kupitia kwenye vikundi vyao.


Vikundi hivyo vya wanawake na vijana vimepokea fedha hizo kwa kipindi cha mwaka 2014/2015 kwa ajili ya kupambana na umaskini na kuijiinua kiuchumi kupitia mfuko wa maendeleo ya wanawake (WDF) na mfuko wa  vijana (YDF).


Mkurugenzi wa halmashauri wa mji wa Korogwe Lewis Kalinjuna wakati akisoma taarifa ya mfuko wa wanawake na vijana mwaka 2014/2015 katika mkutano wa baraza la madiwani uliofanyika mjini Korogwe amesema serikali imekuwa ikitoa mikopo kwa 100% kwa kutumia fedha za makusanyo ya ndani.


“Hakuna fedha yoyote iliyo pokelewa kutoka serikali kuu, halmashauri ya mji imejiwekea utaratibu huu wa kuwapatia wanawake na vijana mikopo kupitia makusanyo yale ya ndani kwa kila mwaka wa fedha,” alisisitiza Kalinjuna.


Amesema fedha zilizotolewa na kukopeshwa kwa vikundi ni mili.60.3 ambapo kiasi kilichokopeshwa kwa vikundi vya wanawake ni sh.mili.40.6 huku vikundi vya vijana vikikopeshwa sh.mili.19.7 na sh.mili.19.7 ikiwa ni ya marejesho ya fedha za mkopo  hadi desemba 2014.


Jumla ya vikundi vilivyokopeshwa ni 106, kati ya hivyo vikundi 72 ni vya wanawake na vijana vikundi 34.


Mkurugenzi huyo amesema katika halmashaurio hiyo mfuko huo umekuwa ukiwanufaisha wanawake na vijana katika kuanzisha na kuendeleza shughuli mbalimbali za ujasiriamali ili kupunguza makali ya maisha na kujiletea maendeleo.

No comments:

Post a Comment