MWANAMKE MAKINI BLOG

Advertise Here

Thursday 29 January 2015

MAJAMBAZI YAPORA MAMILIONI ST. CHRISTINA, YATEKETEZA OFISI


NA PAUL JAMES, TANGA

WATU wasiojulikana wamevamia Ofisi ya Muhasibu katika shule ya St. Christina ya Jimbo katoliki la Tanga iliyopo Kata ya Maweni, Tarafa ya Pongwe na kufanikiwa kuiba fedha tasilim Mil 126 kisha kuichoma moto ofisi hiyo kwalengo lakupoteza ushahidi.



Tukio hilo limetokea Januari 26, mwaka huu katika shule hiyo ambapo mwalimu wa shule hiyo Mary Singano mkazi wa sahare aligundua uvunjifu huo na kutoa taarifa kwa Jeshi la Polisi.



Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo Kaimu Kamanda wa Polisi Juma Ndaki  alisema miongoni mwa fedha ziloibiwa ni pamoja na karo za wanafunzi ambapo mpaka sasa jeshi la polisi lina mshikilia mlinzi wa mahali hapo Jefta Mtiba na wanzanke watano ambao wanatiliwa mashaka.



Aidha Ndaki amesema upelelezi unaendelea kuwabaini watu au mtu aliyehusika na uwizi huo ili hatua zakisheria ziweze kuchukuliwa dhidi yao.



Katika hatua nyingine Askari wa Jeshi la Magereza kutoka Kiwila Mbeya Hermany Nyoni  amefariki dunia papo hapo mara baada ya kuligonga gari aina ya Volvo yenye namba za usajili T408CXB iliyokuwa ikiendeshwa na  Christopher John mwenyeumri wa miaka (38) mkazi wa jijini Tanga  chanzo ikiwa ni mwendo kasi wa pikipiki. 


Kaimu kamanda Ndaki alisema tukio hilo la tarehe 27 Januari majira ya saa 3:30 usiku limetokea katika eneo la Nguzo Tende Kwaminchi Kata ya Nguvumali Tarafa ya Chumbageni barabara kuu ya Tanga-Muheza ambapo   marehemu alikuwa akiendesha pikipiki namba T115CQZ aliligonga gari hilo lililokuwa maegesho kwa nyuma.

No comments:

Post a Comment