MWANAMKE MAKINI BLOG

Advertise Here

Friday 9 January 2015

UELEWA MDOGO BAADHI YA WAJUMBE SERIKALI ZA MITAA WAWAKWAMISHA WENGINE KULA KIAPO


HAFLA ya kuapishwa wenyeviti wateule wa serikali za mitaa wa Halmashauri ya jijini Tanga, imefanyika leo na kukamilika kwa kiwango kikubwa kwenye Ukumbi wa Shule ya ufudi Tanga, iliyopo kata ya Mzingani.
 
Hata hivyo uelewa mdogo miongoni mwa wajumbe hao wa serikali za mitaa, waliopatikana katika uchaguzi uliofanyika hivi karibuni umezua changamoto wakati wa zoezi hilo la kula kiapo hivyo italazimu kurudiwa kwa baadhi yao.
 
Akitangaza utaratibu wa kiapo Hakimu Mkazi Mfawidhi wilaya ya Tanga Aziza Lutalla alisisitiza kuwa kiapo ni kifungo ambacho hakitakiwi kiwe kimefutwafutwa iwe kwa makusudi au kwa bahati mbaya, kauli hiyo ilizua minong’ono kwa baadhi yao hadi pale  alipotangaza kwamba kwa waliokosea kujaza fomu zao za kiapo itawalazimu kurudia kuzijaza upya kisha zitawekwa sahihi nayeye kwa utaratibu utakaopangwa.
 
“Kiapo ni ushahidi wa kukubaliana na masharti ya utumishi wa Umaa katika nafasi yako na kukiuka ni kosa la jinai na kuna adhabu yake kwa mujibu wa sheria za nchi... haitakiwi kiwe kimefutwafutwa, kwahiyo kama kuna mjumbe aliyefanya hivyo awasiliane na mratibu wa zoezi upewe fomu nyingine,” aliwasisitizia viongozi hao
 
Baada ya zoezi la Kuapishwa kwa Wenyeviti 181, wajumbe mchanganyiko 543 na wajumbe 362 wa viti maalumu, Mstaiki Meya wa Jiji la Tanga, Omari Guledi aliwasisitizia viongozi hao kuachana na itikadi za vyama vyao lakini wawe wamoja kwa kufanya vikao kwa mujibu wa taratbu kwa maslahi ya nchi.
 
Nao wajumbe hao walizungumza na Mwanamke Makini walibainishwa kuwa licha ya zoezi hilo kukamilika lakini lilikuwa na dosari ambazo hazina budi kufanyiwa kazi kwa wakati mwengine kwavile sasa limeshapita salama.
 
“Sina hakika kama wajumbe wote wanajua kusoma na kuandika, kama ulifuatilia kwa makini mwandishi wengine hawakuwa wakijaza wala kusema yale maneno ya kuapa, sasa kwasababu tuliapishwa jumla angalau imewabeba," alisema Hussein Abasi  mwenyekiti mtaa wa New Hotel kata ya central

No comments:

Post a Comment